zanglassworks

AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, October 20, 2013

SHILINGI BILIONI 1.2 ZATUMIKA KATIKA UJENZI WA NYUMBA YA SPIKA WA BARAZA LA WAWAKILISHI

Spika wa hivi sasa wa Baraza la Wawakilishi ambae 
atakuwa wa mwanzo kuikaa hii nyumba mpya!

Written by   //  20/10/2013  for Mzalendo Blog

ZANZIBAR.
NYUMBA MPYA YA KISASA YA KUISHI SPIKA WA BARAZA LA WAWAKILISHI IMEKAMILIKA NA ANATARAJIWA KUHAMIA HIVI KARIBUNI MARA BAADA YA KUKAMILIKA KWA MATENGENEZO MUHIMU YA MIUNDOMBINU YA MAJI SAFI.
HAYO YAMEELEZWA NA WAZIRI WA NCHI OFISI YA MAKAMO WA PILI WA RAIS, NDUGU MOHAMED ABOUD MOHD WAKATI AKIJIBU MASWALI YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI KATIKA KIKAO KINACHOENDELEA HUKO MBWENI WILAYA YA MAGHARIBI UNGUJA.
AIDHA WAZIRI ABOUD AMEBAINISHA KUWA NYUMBA HIYO YAKISASA ILIYOPO MIGOMBANI IMEGHARIMU JUMLA YA SHILINGI BILIONI 1.2 AMBAPO ASILIMIA 62 YA FEDHA HIZO ZIMETOLEWA NA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO NA ASILIMIA 18 NI MCHANGO WA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR.
AIDHA WAZIRI HUYO AMESEMA KUWA NYUMBA HIYO IMEKAMILIKA KWA ASILIMIA KUBWA AMBAPO KASORO ZILIZOPO NI TATIZO LA UKOSEFU WA MAJI AMBAPO MIUNDOMBINU HIYO KWA SASA INAFANYIWA MAREKEBISHO.
AMESEMA KUWA NYUMBA HIYO IMEJENGWA KWA KUZINGATIA VIGEZO VYOTE VYA NYUMBA ZINAZOSTAHIKI KUISHI WAKUU WA NCHI.
HATA HIVYO MWAKILISHI WA JIMBO LA WAWI NDUGU SALEH NASSOR JUMA ALISEMA KUWA ENEO ILIPOJENGWA NYUMBA HIYO SIO ZURI KUTOKANA NAKUWEPO BARABARANI AMBAPO UTULIVU UNAKOSEKANA.
AKIJIBU SWALI LA NYONGEZA LA MWAKILISHI HUYO WAZIRI ABOUD AMEFAFANU KUWEPO NYUMBA HIYO BARABARANI SI TATIZO KUTOKANA NA NYUMBA ANAYOISHI RAIS WA ZANZIBAR DK ALI 
Chanzo: Mzalendo
Comments on "SHILINGI BILIONI 1.2 ZATUMIKA KATIKA UJENZI WA NYUMBA YA SPIKA WA BARAZA LA WAWAKILISHI"
fey 20/10/2013 at 6:06 mu · 
  1. Kuwepo barabarani sio tatizo baadaye atafungua milango ya Duka.
    Loh! Hii serikali haina kichwa wala miguu, nyumba ya kukaa spika tuu inagharimu mabilioni ya pesa huku wananchi wanateseka kwa njaa na maradhi. Kwani hivi sasa analala nje? Na kwa nini ajengewe na serikali kwani hana uwezo wa kujenga nyumba yake? Kama ni ulinzi si atapewa akiwa ktk nyumba yake ya private kama watoto wa Shein?
    Haya na ya msaidizi wake ( yule mwanamke) itagharimu ngapi? Hii ndio CCM chukua chako mapema.
  2. Makame Ame 20/10/2013 at 6:20 mu · 
    lnasikitisha kuwa baraza Ietu la kuunda sharia linatumia muda wake kuzungumza upuuzi Kama huu. Tuseme hawana la kuzungumza an wanaogopa ya kuzungumza?
    @ Fey
    Kwa hapa Unguja 1.2 billion si pesa za kusema pesa hasa kwenye ujenzi. Na isitoshe ati 62% zimetoka kwenye Muungano! Na serikali yetu 18% na 20% zinatoka hewani!
  3. makame silima 20/10/2013 at 8:52 mu · 
    MWENYEKITI WA KAMATI ISABU BUNGENI MH ZITTO KAMBWE AENDA ULAYA /USWISS KATIKA HADHINA ZA VIGOGO WA TANZANIA
    Shirika la Kimataifa la Mtandao wa Ulaya wa Madeni na Maendeleo, European Network on Debt and Development (Eurodad) watafanya ziara ya kiuchunguzi kuhusu masuala ya uwazi katika kodi katika nchi za Ulaya kuanzia tarehe 20 Oktoba mpaka tarehe 5 Novemba mwaka 2013.
    Uchunguzi huo utaendeshwa na wataalamu waliobobea wa masuala ya kodi na maendeleo.
    Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali wa Bunge la Tanzania Zitto Zuberi Kabwe ameteuliwa kuongoza Jopo la uchunguzi huo.
    Eurodad ni Mtandao wa Mashirika yasiyo ya kiserikali yapatayo 48 kutoka nchi 19 za Ulaya ambayo yanajihusisha na masuala ya kufutia madeni nchi zilizoendelea, misaada yenye maana na kodi za haki. Mashirika haya yamekuwa kwenye kampeni ya kupinga utoroshwaji wa fedha kupitia ukwepaji kodi unaofanywa na mashirika ya kimataifa kwa nchi zinazoendelea.
    Zitto amekuwa mmoja wa wabunge wanaosimamia hoja ya kutaka Watanzania waliotorosha fedha kwenda nje warejeshe na kufunguliwa mashtaka. Mwaka 2012 aliwasilisha hoja binafsi Bungeni na kupitishwa kuwa Azimio la Bunge ya kutaka uchunguzi kuhusu utoroshwaji wa fedha na kufichwa nje kama Uswiss.
    Kikosi Kazi cha Serikali kutekeleza Azimio hilo la Bunge kinatarajia kuwasilisha taarifa yake katika Mkutano wa Kumi na Sita wa Bunge. Siku ya Jumatatu tarehe 21 Oktoba Zitto atakutana na Waziri wa Fedha wa Uswiss na maafisa wa mabenki na asasi zisizo za kiserikali zilizopo jijini Geneva.
    Pia Zitto atahudhuria mkutano wa Kamati ya Kodi ya Umoja wa Mataifa katika kampeni ya kubadili mfumo wa kodi za kimataifa ili kuzuia unyonyaji wa nchi za Kiafrika unaofanywa na Makampuni makubwa ya Kimataifa.
    Baada ya Geneva Zitto atatembelea nchi za Luxembourg na Brussels kabla ya kwenda Norway ambapo atamalizia ziara yake kwa Jopo la Wataalamu wa masuala ya kodi na Maendeleo kuandika taarifa maalumu yenye mapendekezo kuhusu kuzuia utoroshaji wa fedha kutoka Afrika.
    Zitto atakwenda jijini London kutoa mada kuhusu masuala ya kodi za kimataifa katika mkutano wa Uwazi (Open Government Partnership). Mwenyekiti wa PAC Tanzania atafanya mazungumzo na Mwenyekiti wa PAC Uingereza Bi Margaret Eve Hodge, Lady Hodge MBE, PC, MP kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano wa mabunge mawili na kuendeleza wito wake kwa makampuni ya kimataifa kulipa kodi zao barani Afrika na kuacha tabia ya kutumia ‘Tax Havens’ kukwepa kodi na kufukarisha nchi za Kiafrika.
    CCM NI KUNDI LA WALAJI WA MABILLIONEA KWENDA MBELE.
  4. Bosco 20/10/2013 at 12:32 um · 
    we makame silima si umeshapewa ruhusa ya kuandika mada hapa mtandaoni? sasa kinachokufanya uharibu mada za watu ni kitu gani? au mpak ufungiwe tena uanze kulalamika?
    nikija kwenye mada ikiwa 60% zinatoka ktk serkali ya muungano kumjengea spika nymba ambae blw si mambo ya muungano basi tusitarajie watanganyika kuiachia zanzibar kiurahisi rahisi maana wanatoa gharama kuimarisha muungano.
    @mzee makame ame kila pesa itajwayo weye kwako si nyingi hebu nikuulize pesa nyingi kwako ni tsh ngapi hasa au iwe dola ngapi za kimarekani ndo itakua pesa nyingi kwako?
    inafaa tukaelewa kua budget ya smz ni tsh billion 600 tu sasa unaposema tsh billion 1.5 si pesa mie skuelewi mzee wangu kwa kweli.
  5. fey 20/10/2013 at 12:44 um · 
    @ makame :
    Ni kweli lakini hiyo anayokaa ina tatizo gani? Kuwa serikali igharimike kujenga nyumba mpya ya spika wakati kuna mambo muhimu zaidi.
    Si afadhali ingeshuhulikiwa hiyo Hospitali kwanza? Maana ukienda na moja utarudi na kumi na moja ( maradhi)
    Au kama hawaiwezi na hiyo Hospitali wampe mtu binafsi (iwe private ) kama bandari . Maana imekuwa hizo public service zinauliwa kusudi kwa kuwa wao hawatumii lakini wanasahau kuwa wana ndugu na wazee wao, wanatumia na hata wao huishia humo humo baada ya ulwa.
  6. fey 20/10/2013 at 12:58 um · 
    @ BOSCO:
    Watu wengine wana maradhi pesa hata kama itakuwa kubwa lakini ukiitaja kwa Tsh atadharau lakini itaje kwa dola ya mmarekani hata kama thamani yake ni ya chini mno basi ataona kuwa ina thamani.
    Na kama hiyo asilimia iliyotoka Tanganyika ni kweli basi itakuwa wametukatizia pesa zetu tunazowada. Nadhani itakuwa hivyo au ni tunza wamelipa vibaraka wao wazidi kutukandamiza.
  7. mzaliwa 20/10/2013 at 2:07 um · 
    serikali sio ya zanzibar ila serikali ya ccm zanzibar, kajengewa mtu nyumba za bilioni haya anangapi ambazo alojenga mwenyewe kwa piza za kuiba?
    Panataka kujengwa mnara wa mabilioni wakati maskuli yanaanguka maspitali imekua vituo vya marazi sio vya afya tena,maji hayapatikani wakati wanasema kisiwa kinamaji ndio maana hawajengi nyumba za kwenda juu,hivi kweli serikali ya ccm zanzibar haina muelekeo wala dira.mazumbukuku watupu.
  8. mwandishi 20/10/2013 at 3:17 um · 
    A.aleykum Wazanzibari
    Haya kweli majanga mm nauliza hivi Spika kashakaa muda gani madarakani sasa? Na jee miaka yote alikua anakaa Wapi?Na mshahara na marupurupu aliyokusana hivi hana Nyumba ya kuishi miaka yote hiyo?Na jee hii nyumba iliyojengwa kwa gharama za Serkali ni mali yake?Au ni ya Serkali kwa ajili ya Viongozi? Akistaafu yeye itatumika kwa Kiongozi mwengine au huyo mwengine na yeye atajengewa yake? Kwa kweli inasikitisha saana hii Serkali tulonayo kwa upande wangu mimi naona huu ni msiba mkubwa na Serkali hii yetu HAYA NI MAJANGA.
    NATOWA WITO KWA WALIOKUWA KARIBU NA WAWAKILISHI NA WABUNGE WETU WAULIZE HAYA MASUALI HUU NI MCHOZO MCHAFU SANA NA UNAKIRIHISHA HII NI AIBU KWA VIONGOZI WA NCHI NA SERKALI.
    MAASALAM.

No comments :

Post a Comment