NA MWANDISHI WETU
22nd October 2013
Hayo yalisemwa juzi na Rais wa kampuni hiyo, William Xu wakati wa mazungumzo na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwenye makao makuu yake jijini Shenzhen, China.
Alisema walipokea maombi ya serikali ya Tanzania ya kusaidia Mkongo wa Mawasiliano ya Taifa (NCITBB) ili kuinua kiwango cha elimu ya watoto wa Kitanzania. Kampuni ya Huawei ndiyo iliyojenga mkongo huo.
Alisema kwa kuanzia, mradi huo utazihusu shule 50 ambapo shule mbili kutoka kila mkoa zitaunganishwa kwenye mtandao zikiwa na madarasa ya kujifunzia teknolojia mpya (multimedia classrooms), maabara ya kompyuta (computer lab), projekta, mafunzo ya kwenye mtandao yanayofundishwa kwa njia ya video, (Online video teaching) na (online applications).
“Shule nyingine 100 zimekwishaainishwa lakini zenyewe hazitakuwa mtandaoni moja kwa moja, bali katika awamu ya pili zinaweza kuunganishwa na kuwa mtandaoni kutegemea na upatikanaji wa intaneti na kasi yake.
CHANZO: NIPASHE
No comments :
Post a Comment