dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, September 11, 2014

DMV USA: MGOGORO WA HUJUMA ZIDI YA JUMUIYA YA WATANZANIA ATC-METRO WAELEKEA KUCHUKUA SURA MPYA

  • WASHINGTON DC ATTORNEY GENERAL KUINGILIA KATI. 
  • ANAMAMLAKA KISHERIA KUCHUNGUZA  UFISADI
  • WATAKAOBAINIKA KUITUMIA JUMUIYA KWA MASLAHI BINAFSI KUCHUKULIWA HATUA KALI ZA KISHERIA.
  • IRS KUSHIRIKI KATIKA UCHUNGUZI HUO

             Bodi Memba wa ATC akimtisha Libe kwa kumtumbulia macho katika mkutano wa juzi!

Mgogoro ulioikumba jumuiya hii baada ya wachache kuitumia kwa maslahi binafsi umechukua sura mpya baada ya Attorney General wa Washington DC ilikosajiliwa jumuiya hii na mwenye mamlaka kisheria ya udhibiti wa jumuiya kama hizi kufanya kazi yake ya uchunguzi zidi ya ubadhirifu na ufisadi unaozikumba jumuiya, taasisi za kidini na vikundi mbalimbali vilivyosajiliwa chini yake kwa chatter ya " for nonprofit organization and 501(3)c - Tax Exemption". Hali imekuwa sugu kwa vikundi vingi na wahusika wa ubadhirifu wameshitakiwa na kupewa hadhabu kali sana pamoja na vifungo kati ya mwaka mmoja na kuendelea. Moja ya mashariti ya usajiri wa jumuiya hizi ni kuzingatia kanuni na sheria zinazotoa muongozo wa kazi zake, hivyo kutozifuata upelekea jumuiya kufungiwa na watekelezaji wake kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.
Vijana wa kikundi cha Nyarugusu wakiwa kazini!

Uongozi unawajibika kuwajulisha wanachama taarifa za fedha na miradi iliyopo, pia kutunza kumbukumbu na kuwaziweka wazi kwa wanachama wakati wote.
Pia ni wajibu wao kuipa taarifa mara kwa mara ofisi ya Attorney General ili kudumisha usajiri wa jumuiya husika. Taarifa za mapato na misamaha ya kodi hupelekwa Idara ya kodi IRS sharti muhimu ili jumuia husika iendelee kuwa na kibari cha msamaha wa kodi "Tax Exemption for nonprofit making Organization/Corporation" kanuni ijulikanayo kama 501(c) 3. Hatua hii itamaliza mzizi wa fitina na kusafisha wale wote waliohusika kuihujumu jumuiya kwa kipindi kirefu. Watu hawa wametumia mbinu maksudi kuwagawa wanachama kidini, kiitikadi, kuwazuia wanachama kuona rekodi za mikutano, miradi na fedha.

Kutozingatia miongozo ya kikatiba, hujuma zidi ya haki za wanachama kuchagua na kuchaguliwa katika uongozi ngazi mbali mbali. Kukaa madarakani zaidi ya muda kikatiba, matumizi mabaya ya fedha. Matumizi ya jina la jumuiya katika mitandao binafsi ya kibiashara. Pia wachache hawa wamejaribu kujadiri mabadiriko ya katiba nje ya utaratibu kikatiba. Wameficha "Bylaws" document muhimu inayotafsiri katiba ili wanachama wasijue haki zao ndani ya jumuiya. Watu hawa mahamuma wametishia kutumia vikao haramu kuwasimamisha hata kuwafukuza uanachama wale wote waliohoji na kukemea uvunjwaji wa katiba ili waendelee kuihujumu jumuiya. Wamediriki hata kuwataka hawa wapigania haki waanzishe jumuiya yao.
Hatua ya baadhi ya wanachama kwenda mahakamani na sasa wengine kumuhusisha Attorney General itakuwa ni hatua muafaka katika kutatua mgogoro huu uanaozidi kukomaa kila kukicha na itakuwa fundisho kwa vizazi vijavyo na wale wachache wanaopenda kuishi nchini hapa kwa kutumia migongo ya walio wengi ili kusukuma agenda ovu ya ufisadi.
Chanzo: Swahilivilla

No comments :

Post a Comment