dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, September 10, 2015

Wasomi, wanaharakati wamshukia Gwajima

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima.
Dar es Salaam. Baada ya Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima kuibua mambo mazito ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa juzi, wanaharakati na wasomi wametoa maoni yao na kueleza kusikitishwa na hatua za kiongozi huyo wa dini kutoa siri za waumini wake.
Wanaharakati hao pia wameiomba serikali ipige marufuku viongozi wa dini kujihusisha na siasa.
Juzi, Gwajima alizungumza na wanahabari Dar es Salaam, alisema Dk Slaa amestaafu siasa kwa sababu ya shinikizo la mkewe, Josephine Mushumbusi.
Kiongozi huyo machachari wa dini katika mazungumzo yake na waandishi wa habari, alipinga kauli iliyotolewa na Dk Slaa, kwamba amejiuzulu siasa kwa sababu chama chake kimekiuka makubaliano kwa kumkaribisha Edward Lowassa.
Kadhalika, Gwajima alikwenda mbali na kudai Mushumbusi alimfukuza na kumrushia Dk Slaa nguo zake, akimtaka ajiuzulu Chadema hali iliyosababisha katibu mkuu huyo wa zamani kulala ndani ya gari.
Gwajima aliyasema hayo wakati Dk Slaa na familia yake wakiwa safarini kuelekea Marekani kwa mapumziko, huku akisema kurejea kwake kutategemea mazingira ya wakati husika. Dk Slaa aliaga kupitia Televisheni ya Azam katika mahojiano maalumu.
Wasomi na wanaharakati
Aliyekuwa Mkuu wa Chuo Kikuu Huria (OUT), Profesa Tolly Mbwete aliwataka Gwajima na Dk Slaa kuachana na masuala ya kupambana kwenye majukwaa, badala yake aliwataka waongelee masuala ya maendeleo.
“Hao wazee waachane na hayo mambo, ni mfano mbaya kwa vijana. Waongee masuala ya kimaendeleo, wanatutia aibu sisi wazee wenzao,” alisema.
Mkazi wa Magumuchila, Masasi mkoani Mtwara, Julius Mazinde alisema vita hiyo ya maneno kati ya watu wawili ambao ni viongozi wa kiroho, inatia shaka na inatishia amani ya nchi.
“Unajua Gwajima ana wafuasi na Dk Slaa ana wafuasi wengi, haya malumbano yao yakizidi, wanaweza kufika pabaya ikaleta machafuko, lakini sisi tunaombea hilo lisitokee,” alisema.
Mazinde alimsihi Gwajima kukaa kimya iwapo Dk Slaa atajibu lolote, pia, alimuomba Dk Slaa asijibu chochote ili kuepusha kuchochea malumbano zaidi.
Serikal ipige marufuku
Kuhusu viongozi wa dini kutoa siri za waumini wao, kwa mfano Gwajima alipotamka kuwa Mushumbusi ana mapepo, Mkufunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Dk Eliamani Sedoyeka aliishauri Serikali kupiga marufuku viongozi wa dini kujiingiza katika siasa.
Alisema imekuwa bahati mbaya kuwa viongozi wetu wanachanganya siasa na dini, hali ambayo aliitaja kuwa ni kufilisika.
“Kikubwa mimi sioni kama kutaja zile siri za Dk Slaa kuna mashiko, kwanza Serikali haiamini kuhusu mapepo, haina dini,” alisema.
Alizungumzia pia malumbano ya Dk Slaa na Chadema na kusema hatua zinazofikiwa na baadhi ya viongozi hao, zinawakatisha tamaa wananchi na kuleta taswira mbaya kwa wapiga kura wao.
Alimtaka Askofu Gwajima afute usemi wake kuhusu Dk Slaa na kumsihi Dk Slaa ajisafishe kuhusu tuhuma zake kwa maaskofu.
Akizungumzia hilo, Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo Bisimba alisema kutokana na nafasi ya Gwajima nchini, yaani uaskofu, hakutakiwa kutoa siri za Dk Slaa, bali alitakiwa kujikita kujibu hoja za kuitwa mshenga, kujibu kama amehongwa au hakuhongwa na kujibu tuhuma za maaskofu.
“Kimaadili si vizuri kutoa siri hizo, angeweza kujibu bila kutaja mambo mengine kama masuala ya mapepo, kutokana na nafasi yake si vizuri alivyofanya”alisema.
Alisema kuwa Gwajima alikwenda kinyume na maadili ya kazi yake ya utumishi wa Mungu kwani si jambo jema kueleza siri za muumini kuwa anamapepo.
Maswali kwa Gwajima
1. Kwa nini walinzi wa Gwajima wanamlinda Dk Slaa? Je, Gwajima ana kampuni ya ulinzi.
2. Gwajima anamiliki silaha ngapi? Ni silaha za aina gani? Na kwa nini amiliki silaha nyingi?
3. Kwa nini anatoa siri za waumini wake kuwa wana mapepo?
4. Kwa nini alikuwa anarekodi kila kitu alichozungumza na Mushumbusi na Dk Slaa?
5. Je, kuna utata wa tarehe ya ujumbe mfupi uliyotumwa na Dk Slaa kwa Gwajima na tarehe ya Lowassa kuondoka CCM.
6. Kwa nini ana ulinzi mkubwa unaotia shaka?
/Mwananchi.

No comments :

Post a Comment