Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakary Zubeiry bin Ally. Picha ya Maktaba.
Dar. Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) leo limemchagua Sheikh Abubakary Zubeiry bin Ally kuwa Mufti Mkuu wa Tanzania.
Katika uchaguzi huo uliofanyika leo kwenye Ukumbi wa Africa Dream mjini Dodoma, Tume ya Dini ya Kiislamu imemchagua Sheikh Zubeiry kwa kura 310 za ndiyo baada ya kuingia kwenye uchaguzi huo akiwa mgombea pekee.
Akitangaza matokeo hayo, Mwenyekiti mstaafu wa Halmashauri Kuu ya Bakwata, Alhaji Habib Ndassiwa amewataja wagombea waliojitoa kuwa ni Sheikh Ally Muhidini Mkoyogole, Sheikh Hamis Abbas Mtupa na Sheikh Hassan Ibrahim Kiburwa.
Mufti Zubeiry aliteuliwa kukaimu nafasi hiyo ya juu katika dini ya Kiislamu mnamo Juni 22 mwaka huu baada ya kifo cha Mufti Issa Shaaban Simba kilichotokea katika Hospitali ya TMJ jijini Dar es Salaam alikokuwa amelazwa kwa matibabu.
Alitakiwa kushikilia nafasi hiyo kwa muda wa miezi mitatu (Siku Tisini) hadi Septemba mwaka huu kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa kujaza nafasi hiyo.
No comments :
Post a Comment