Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, November 3, 2015

Viongozi Wakuu EAC, Sadc kushuhudia Magufuli akiapa.

Rais Mteule, Dk. John Magufuli.
Viongozi Wakuu kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), na wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc), wamethibitisha kuhudhuria sherehe za kumuapisha Rais Mteule, Dk. John Magufuli keshokutwa jijini Dar es Salaam.
 
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula, aliyasema hayo jana wakati akizungumza na Nipashe kuhusu maandalizi ya kuwapokea wageni mbalimbali kutoka nje ya nchi wanaotarajia kuhudhuria sherehe hiyo.
 
“Mialiko imeshakwenda, lakini mpaka sasa hakuna aliyewasili, ila tumeshaanza kupokea majibu ya viongozi mbalimbali wa kanda kuwa watafika katika sherehe hiyo,” alisema Balozi Mulamula.
 
Alisema nchi jirani kama Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kenya, Uganda, zimethibitisha kushiriki sherehe za kumuapisha Dk. Magufuli. Alisema orodha kamili na idadi ya wageni watakaokuja, bado haijapatikana, lakini Wizara imeshajiandaa kupokea idadi yoyote ya wageni watakaokuja.Alisema licha ya Ofisi ya Waziri Mkuu kusimamia sherehe hiyo, lakini Wizara nayo imejipanga katika suala zima la malazi kwa wageni watakaofika nchini.
 
Aliongeza kuwa pia wanatarajia kupokea wageni kutoka China, nchi za Nordic, Marekani na Uholanzi.
 
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment