Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, November 4, 2015

Wagombea urais wa Zanzibar waondolewa ulinzi!

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (Zec), Jecha Salum Jecha
Wagombea wa nafasi ya urais Zanzibar wameondolewa ulinzi siku moja  baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (Zec) kufuta matokeo  ya uchaguzi mkuu wa visiwa hivyo.
 
Uchunguzi wa Nipashe umebaini kuwa, wagombea 12 waliokuwa wakiwania  nafasi hiyo wameondolewa ulinzi wa askari kanzu (polisi) waliokuwa  wakiwalinda tangu walipoteuliwa na Zec kuwa wagombea.
 
Wagombea walionyang’anywa ulinzi ni Khamis Iddi Lila (ACT-Wazalendo),  Juma Ali Khatib (Tadea), Hamad Rashid Mohammed (ADC), Soud Said Soud  (AFP), Ali Khatib Ali (CCK), Mohammed Masoud Rashid (Chaumma) na Tabu  Mussa Juma (Demokrasia Makini).
 
Wengine ni Abdallah Kombo Khamis (Demokratic Party), Kassim Bakari  Ali (Jahazi Asilia), Seif Ali Iddi (NRA), Issa Mohammed Zonga (Sau)  na Hafidh Hassan Suleiman (TLP).
 
Wagombea waliobakia na ulinzi kutokana na nyadhifa zao ni Rais wa  Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein na Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim  Seif Sharif Hamad.
 
Mgombea wa urais wa Jahazi Asilia,  Kassim Bakar Ali alisema haikuwa  muafaka kwa wagombea wa urais kuondolewa ulinzi wakati uchaguzi bado  haujakamilika na mshindi kupatikana.“Sisi bado ni wagombea na hatujapokea barua yoyote ya kufutwa  kugombea kwetu, tunachosubiri uchaguzi ukamilike inakuaje tuondolewe  ulinzi?” Alihoji mgombea huyo.
 
Alisema tangu matokeo ya uchaguzi wa Zanzibar yafutwe, wagombea wote  wamebakia njiapanda hawafahamu kinachoendelea kutokana na Tume ya  Uchaguzi kukaa kimya.
 
“Huwezi kuwaondolea wagombea ulinzi kabla ya fainali ya mchezo  haijamalizika, sisi ni wagombea na kama itatokea mmoja wetu  kuhujumiwa na kupoteza maisha uchaguzi utalazimika kuahirishwa,”  alisema mgombea Juma Ali Khatib wa Tadea.
 
Alisema mlinzi aliyepewa alimuaga ghafla kuwa hawatakuwa pamoja  anarudi kuendelea na shughuli nyingine kazini baada ya matokeo ya  uchaguzi kufutwa.
 
Alisema Zec inapaswa kukaa pamoja na wagombea wote kuwaeleza nini  kinachoendelea badala ya kukaa kimya kwa zaidi ya wiki moja sasa bila  ya kutoa taarifa yoyote tangu kufutwa kwa matokeo hayo.
 
Kamishna wa Polisi Zanzibar, Hamdan Omar Makame, alithibitisha  wagombea hao kuondolewa ulinzi baada ya tume kufuta matokeo ya  uchaguzi Zanzibar Oktoba 28, mwaka huu.
 
Alisema ulinzi huo utarejeshwa baada ya Tume ya Uchaguzi kutoa  utaratibu na ratiba ya uchaguzi wa marudio.
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment