Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, November 4, 2015

CCM wajiandaa na uchaguzi wa marudio Zanzibar!

Yussuf Mohammed
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimeanza kuwaandaa wanachama wake  na uchaguzi wa marudio baada ya Tume ya Uchaguzi visiwani humo (Zec)  kufuta matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25, mwaka huu.
 
Akizungumza na wanachama wa CCM mkoa wa Magharibi, Mwenyekiti wa  chama hicho mkoani humo, Yussuf Mohammed, aliwataka wanachama hao  kushiriki uchaguzi wa marejeo.
 
“Msione ajabu kushiri uchaguzi wa marejeo CCM itashinda kwa kishindo  kikubwa ni kujipanga na kujiandaa vizuri kushiriki uchaguzi huo, tume  ikisema kesho uchaguzi unarejewa sisi ni kwenda kupiga kura tu,”  alisema.
 
Akizungumza na wanachama wa CCM tawi la Kiembesamaki, alisema CCM  mkoa wa Magharibi inaunga mkono tamko la serikali lililotolewa na  Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi kuwa wananchi watulie na  wasubiri uchaguzi wa marejeo ili kwenda kupiga kura.
 
Aliwataka wana-CCM kuwa makini na kupuuza propaganda kuwa CCM  inafanya njama ili kushinda uchaguzi huo.
 
Alidai kuna maandalizi yanayofanywa na vyama vya upinzani kusambaza  vipeperushi ambavyo vinasomeka kuwa Dk. Ali Mohammed Shein ameridhia  Maalim Seif Sharif Hamad  (Cuf) atangazwe kuwa mshindi wa urais wa  Zanzibar wakati uchaguzi uliofanyika  Oktoba 25 ulikuwa na  udanganyifu mkubwa.
 
“Niwaombe wana-CCM vipeperushi hivyo karibu vitasambazwa mitaani  lakini ukishakipata kisome halafu kichome moto wala usihadaike,”  alisema.
 
Mohammed alitoa wito kwa wananchi wakiwamo wana-CCM kuwa watulivu na  kudumisha amani na kutokubali kushawishiwa kuivuruga amani iliyopo. 

CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment