dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, December 15, 2015

Mradi wa umeme Kinyerezi ukamilike Januari - Waziri

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Medard Kalemani
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Medard Kalemani, amelitaka Shirika la Umeme nchini (Tanesco) kukamilisha mradi wa uzalishaji umeme kwa kutumia gesi wa Kinyerezi I ifikapo Januari, mwakani ili nchi iwe na umeme wa uhakika.
 
Naibu Waziri alitoa maagizo hayo baada ya kufanya ziara kwenye mitambo hiyo eneo la Kinyerezi jijini Dar es Salaam jana akiwa amefuatana na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Omar Chambo na watendaji wengine wa Wizara ya Nishati na Madini na Tanesco.
 
Dk. Kalemani alitoa agizo hilo baada ya watalaam wa Tanesco wanaosimamia mradi huo kumueleza kuwa kwa sasa kituo hicho kinazalisha umeme wa megawati 70 kati ya megawati 150 na kwamba megawati 80 zilizobaki zitakuwa tayari ifikapo Februari, mwakani.
 
“Kwa sasa tunazalisha megawati 70 kati ya 150, hizi hazitoshi, tujitahidi kuzalisha zaidi ya hizi kabla ya Februari, kwani wananchi wamechoka na hili suala la ukatikaji wa umeme wa mara kwa mara, mmesema gesi ipo ya kutosha, hivyo lazima mitambo izalishe umeme kama inavyotakiwa,” alisema Dk. Kalemani.
 
Awali, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Omar Chambo, alimweleza Naibu Waziri kuwa mitambo miwili kati ya minne, ndiyo inayofanya kazi eneo hilo la Kinyerezi I na kuzalisha megawati 70 zinazoingizwa katika gridi ya Taifa.
 
Alieleza kuwa kwa sasa serikali imeamua kujenga mitambo mingine ya kuzalisha umeme katika eneo hilo (Kinyerezi I Extension) ambayo itakuwa na uwezo wa kuzalisha megawati 185 ili nchi iwe na umeme wa uhakika unaotokana na nishati ya gesi asilia.
 
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment