dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, December 15, 2015

Diwani Chadema azusha kizaazaa Njombe

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)  mkoani hapa kimeingia katika sintofahamu, baada ya Diwani wa Viti Maalumu aliyeteuliwa kutoka Jimbo la Linguini kuwekwa katika jimbo ambalo si lake.
 
Wanachama wa chama hicho waliingia katika sintofahamu baada ya diwani wa chama hicho kutoka Jimbo la Lupembe kupewa kiti maalumu katika Jimbo la Njombe Kusini.
 
Akitoa ufafanuzi wa jambo hilo ambalo limeleta taharuki na kulalamikiwa na baadhi ya wanachama wa Chadema, Mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Njombe, Alatanga Nyagawa, alisema chama hicho kimeingia katika mvutano kuhusiana na suala hilo na kuwaomba wanachama kuwa na utulivu wakati likishughulikiwa.
Alisema jambo hilo huenda lilifanyika ngazi ya taifa idara ya wanawake ya chama hicho, kwa kuwa majina yote yalipelekwa huko na uchambuzi ulifanyika na kutumwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec).
 
Alisema kama kosa hilo alikufanyika katika chama ngazi ya taifa, litakuwa limefanyika Nec ambako majina hayo yalitumwa.
 
Nyagawa alisema jambo hilo linaweza kufanywa na chama chochote, kwani limetokea kwa bahati mbaya.
 
Aliwaomba wafuasi wa chama hicho kuwa watulivu wakati suala hilo linashughulikiwa na uamuzi utatolewa na kwamba ikibainika kuna kosa limefanyika, huenda akanyang'anywa udiwani na kupewa mtu wa chama hicho Jimbo la Njombe Kusini.
 
Diwani huyo alipata shida wakati wa kuapa kutokana na kuwa na wasiwasi na kushindwa kutamka kile kilicho kuwa kimeandikwa katika karatasi ya kiapo.
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment