dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, May 20, 2017

Serikali yaanza mazungumzo ya ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta!

Serikali ipo katika hatua ya mazungumzo ya ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta masafi kutoka Dar es Salaam hadi Ndola Zambia, litakaloenda sambamba na bomba la TAZAMA, ili kuondoa tatizo la uharibifu wa barabara nchini, unaosababishwa na usafishwaji wa mafuta kwa njia ya magari.

Akipokea ripoti ya utendaji wa sekta ndogo ya petroli kwa mwaka 2016, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo, Kaimu Mkurugenzi wa Sekta ya Mafuta katika wizara hiyo Eng. Innocent Lwoga amesisitiza kuwa mradi huo umekusudiwa kukamilika kabla ya mwaka 2020.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya bunge ya Nishati na Madini Bw. Doto Biteko amewashauri wafanyabiashara ya mafuta kushirikiana na vyombo vya serikali, huku Mkurugenzi Mtendaji wa (EWURA) Bw. Felix Ngamlagosi akisisitiza kuwa mamlaka yake inatafutiwa ufumbuzi juu ya suala la kuwepo kwa viwango vya gesi ya kupikia nchini, kama ilivyo kwa nchi nyingine duniani.

No comments :

Post a Comment