dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, October 6, 2017

Ester Bulaya: Niko hatarini!



Mbunge wa jimbo la Bunda Mjini kupitia tiketi ya CHADEMA, Ester Amos Bulaya, amesema yupo katika hatari kubwa kutokana na kufuatiliwa na watu ambao anahisi sio wazuri huku wakiwa wamevalia mavazi ya ninja, nyumbani kwake wilayani Bunda.

Bulaya ameto taarifa hiyo alipokuwa akiongea na mwandishi wa East Africa Television, na kusema kwamba watu hao walimfuata nyumbani kwake wakiwa na gari ya Noah huku wamevalia kinija, bahati nzuri hakuwepo nyumbani hivyo ndugu zake wakamwambia asirudi  nyumbani siku hiyo.

Ester Bulaya ameendelea kuelezea kwamba watu hao walizunguka kwa baadhi ya ndugu zake akiwemo bibi yake na kumkosa, lakini alienda kutoa taarifa polisi na mkuu wa kituo kuanza kufuatilia suala hilo, lakini haikuchukua muda akahamishwa kituo cha kazi.

/ EATV

No comments :

Post a Comment