zanglassworks

AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, November 10, 2017

Urusi kulipiza kisasi hatua ya Mrekani!

Urusi inajiandaa kulipiza kisasi dhidi ya hatua ya Marekani ya kuagiza shirika la utangazaji la RT kujiandikisha kama "ajenti wa kigeni".

Urusi inapanga kulipiza kisasi dhidi ya mashirika ya utangazaji ya Marekani.

Mmoja wa wabunge wenye ushawishi mkubwa mwenye uhusiano na ikulu ya rais wa Urusi amesema nchi hiyo itachukua "hatua pana" ambazo "huenda zikahusisha mitandao mingi ya kijamii".

RT imetajwa kama chombo cha habari cha propaganda huku tuhuma za Urusi kuingilia uchaguzi wa Marekani wa mwaka jana zikiendelea.CNN, Sauti ya Amerika (VoA) na Radio Free Europe/Radio Liberty yametajwa kama mashirika ambayo huenda yakaandamwa na Urusi.

Seneta wa urusi anayehusika katika sera ya vyombo vya habari Alexei Pushkov amesema mashirika hayo ya habari ya Marekani "yanafaa kuwekewa masharti ikiwa ni pamoja na huduma zake za runinga."

Sergei Neverov, kiongozi wa chama cha United Russia - chenye uhusiano wa karibu na serikali ya Urusi - bungeni, amesema "sio tu kwamba tutaandika mapendekezo, bali pia tume itaandaa mikakati pana, ambayo huenda ikahusisha mitandao ya kijamii."

Awali, RT kupitia taarifa walikuwa wamesema Wizara ya Haki ya Marekani ilikuwa imelipa shirika hilo hadi Jumatatu kujiandikisha kama ajenti wa kigeni la sivyo wakuu wa shirika hilo wakabiliwe na hatari ya kukamatwa na kwamba akaunti zake za benki huenda zikazuiliwa.

Maagizo hayo yametolewa chini ya Sheria ya Kuwasajili Maajenti wa Kigeni (FARA), iliyopitishwa 1938 kukabiliana na kuenea kwa itikadi za Kinazi nchini Marekani.

No comments :

Post a Comment