dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, September 29, 2018

CCM yawaonya makada wake wanofanya kampeni kurithi nafasi ya Rais Shein!


Kamati kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) taifa kimewaonya baadhi ya makada na wanachama wake ambao wameanza shughuli za kampeni kwa ajili ya kurithi nafasi ya Rais wa sasa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt Ali Mohamed Shein kwa madai jambo hilo ni kinyume na taratibu a chama hicho.

 Kupitia taarifa iliyotolewa na chama hicho kupitia kikao maalum cha kamati kuu kilichoketi leo septemba 29 imesema "inatoa karipio la mwisho kwa wana CCM, kwa kukiuka kanuni za uchaguzi kwa kufanya kampeni za kificho na za wazi za Urais wa Zanzibar na kwenda kinyume na kanuni na chama hicho."

Aidha Chama hicho kimepitisha jina la Ramadhani Hamza Chande kuwania nafasi ya uwakilishi visiwani humo katika jimbo la Jang'ombe.

Aidha Chama hicho kimepitisha jina la Ramadhani Hamza Chande kuwania nafasi ya uwakilishi visiwani humo katika jimbo la Jang’ombe kufuatia hatua ya chama hicho kumvua uanachama aliyekuwa Mwakilishi wa jimbo hilo Abdalla Diwani kwa tuhuma mbalimbali.

Kikao hicho cha kamati kuu maalum ya Halmashauri kuu ya CCM (NEC) kiliendeshwa na Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa ambae pia n Rais wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe M,agufuli.

No comments :

Post a Comment