Naibu Waziri wa Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee ,Wanawake na Watoto, Shadya Mohamed Suleiman amewataka wanafunzi wa jimbo la Magomeni kushughulika masomo na kujiepusha tamaa.
Hayo ameyasema leo katika ukumbi wa skuli ya Maandalizi ilioko Jimbo la Magomeni wakati wa sherehe ya utoaji wa zawadi kwa wanafunzi waliofaulu kuingia michepuo , kidato cha pili na kidato cha tano kwa mwaka 2017/2018.
Amesema ili wafanikiwe zaidi katika elimu ni lazima wawe wasikivu na wavumilivu kwa kufuata ushauri wa walimu ndipo watafanikiwa kwani elimu ndio mustakabali mzima wa maisha na kuwataka waongeze bidii katika masomo kwani wao ndio wataalamu watarajiwa wa hapo baadae.
“Wacheni tamaa za kutamani vitu ambavyo wazazi hawana uwezo navyo mambo haya ndio yanayoweza kukuharibieni malengo yenu mliojiwekea ya baadae shuhulikieni masomo yenu”, alisema Naibu huyo.
Vile vile, Shadya amewapongeza watoto wa kike kwa kufaulu wengi na kuwataka waache ukimya pale wanapokabiliwa na vitendo vya udhalilishaji kwa kuwaripotia wazee wao ili sheria zichukuliwe kwa haraka.
Aidha aliwataka walimu kuongeza bidii kwa kuwa karibu na wanafunzi ili kuwashajihisha na Serikali inawaandalia walimu mazingira mazuri na kuwaondolea changamoto zinazowakabili.
Pia aliwaasa wazee kufata nyendo za watoto wao na kuwataka kuwa karibu nao kila wakati kwani vitendo vya ushalilishaji vinazidi kushamiri hasa kwa wanawake na watoto pamoja na wanafunzi .
“Vitendo vya udhalilishaji vipo hivyo wazazi wenzangu tujitahidi kuwa na watoto wetu kila wakati ili kuzijua nyedo zao za kila siku, na ukimuona ana kitu cha thamani tusiogope kuwauliza na kufatilia wapi kapata”, alisema Shadya.
Nae Mbunge wa Jimbo hilo Jamal Kassim na Mwakilishi Rashid Shamsi Makame wamesema wameanza kutoa zawadi hizo tangu walipoanza kuingia madarakani , huu ni muendelezo na wameahidi kuendelea kutoa zawadi hizo kwa kila wanaofaulu ili kuwajengea hamasa na kuzidisha bidii katika masomo yao ikiwa ni ahadi zao walizoziahidi.
Wakitoa wito kwa wazee na walimu kuwa na mashirikiano kwa lengo la kuona vijana hao wanafikia nafasi nzuri kielimu kwani duniani kote sasa elimu ndio inoleta maendeleo na mafanikio hayawezi kupatikana iwapo watakosekana wasomi.
Hayo ameyasema leo katika ukumbi wa skuli ya Maandalizi ilioko Jimbo la Magomeni wakati wa sherehe ya utoaji wa zawadi kwa wanafunzi waliofaulu kuingia michepuo , kidato cha pili na kidato cha tano kwa mwaka 2017/2018.
Amesema ili wafanikiwe zaidi katika elimu ni lazima wawe wasikivu na wavumilivu kwa kufuata ushauri wa walimu ndipo watafanikiwa kwani elimu ndio mustakabali mzima wa maisha na kuwataka waongeze bidii katika masomo kwani wao ndio wataalamu watarajiwa wa hapo baadae.
“Wacheni tamaa za kutamani vitu ambavyo wazazi hawana uwezo navyo mambo haya ndio yanayoweza kukuharibieni malengo yenu mliojiwekea ya baadae shuhulikieni masomo yenu”, alisema Naibu huyo.
Vile vile, Shadya amewapongeza watoto wa kike kwa kufaulu wengi na kuwataka waache ukimya pale wanapokabiliwa na vitendo vya udhalilishaji kwa kuwaripotia wazee wao ili sheria zichukuliwe kwa haraka.
Aidha aliwataka walimu kuongeza bidii kwa kuwa karibu na wanafunzi ili kuwashajihisha na Serikali inawaandalia walimu mazingira mazuri na kuwaondolea changamoto zinazowakabili.
Pia aliwaasa wazee kufata nyendo za watoto wao na kuwataka kuwa karibu nao kila wakati kwani vitendo vya ushalilishaji vinazidi kushamiri hasa kwa wanawake na watoto pamoja na wanafunzi .
“Vitendo vya udhalilishaji vipo hivyo wazazi wenzangu tujitahidi kuwa na watoto wetu kila wakati ili kuzijua nyedo zao za kila siku, na ukimuona ana kitu cha thamani tusiogope kuwauliza na kufatilia wapi kapata”, alisema Shadya.
Nae Mbunge wa Jimbo hilo Jamal Kassim na Mwakilishi Rashid Shamsi Makame wamesema wameanza kutoa zawadi hizo tangu walipoanza kuingia madarakani , huu ni muendelezo na wameahidi kuendelea kutoa zawadi hizo kwa kila wanaofaulu ili kuwajengea hamasa na kuzidisha bidii katika masomo yao ikiwa ni ahadi zao walizoziahidi.
Wakitoa wito kwa wazee na walimu kuwa na mashirikiano kwa lengo la kuona vijana hao wanafikia nafasi nzuri kielimu kwani duniani kote sasa elimu ndio inoleta maendeleo na mafanikio hayawezi kupatikana iwapo watakosekana wasomi.

No comments :
Post a Comment