Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, November 6, 2019

ZANZIBAR: SMZ yaiomba UNICEF kufanya utafiti wa utapiamlo kwa Watoto!

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeliomba Shirika la kuhudumia watoto Duniani UNICEF kufanya utafiti juu ya hali ya utapiamlo kwa watoto  ambao wanakumbwa na tatizo hapa nchini

 Ombi hilo limetolewa na Waziri wa Afya Zanzibar Hamadi Rashid Mohamed huko Ofisini kwake  wakati akizungumza na Mwakilishi mkazi wa Shirika hilo kanda ya Zanzibar Maha Damaj, amesema Zanzibar imekuwa na uzalishaji mkubwa wa chakula, matunda na mboga mboga lakini bado kumekuwa na ongezeko la tatizo hilo nchini.
Alisema  tatizo la utapiamlo huwaathari watoto wengi kutokana na kukosa vyakula vyenye afya ambalo limeonekana katika vituo vya afya na skuli.

Alisema ipo haja ya kufanya utafiti ili kujua njia ya kuondosha tatizo hilo pamoja na kuelimisha jamii juu ya madhara  na kuwakinga watoto na madhara hayo.

“Watoto ndio taifa la kesho hivyo ipo haja yakuona wanakuwa vizuri  kwa kupata  vijana wenye afya na kulitumikia taifa lao badae”, alieleza Waziri Hamad.
Waziri Hamad alisema maeneo yaliyoathirika zaidi na tatizo hilo ni Wilaya Micheweni kwa upnde wa Pemba na Mkoa wa Kaskazini Unguja ni maeneo ambayo yameonekana kutokea kwa vifo vingi vya kinamama na watoto.

Nae Mwakilishi Mkazi Bi Maha Damaj  Shirika lake litalishughulikia suala na kufanya utafiti na  kuhakikisha kwamba wanalipatia ufumbuzi na kujua sababu ya tatizo hilo katika maeneo hayo.

Aidha alisema kuwa yupo tayari kuitangaza Zanzibar na kuifanya kuwa ni kituo cha elimu ya malaria kutokana na mafanikio makubwa ya kutokomeza maradhi hayo kwa asilimia 0.2 jambo ambalo ni faraja kubwa duniani.

Hata hivyo Muwakilishi huyo alisema kuwa shirika lake litatoa vifaa vya kina mama na watoto katika vituo vya afya 36 vya Unguja na Pemba.

No comments :

Post a Comment