dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, June 26, 2020

Ubalozi Wa Marekani Watoa Tamko Kuelezea Masikitiko Yao Kuhusu Uhuru wa Kujieleza na Ushiriki Jumuishi wa Kisiasa Nchini Tanzania!


Ubalozi wa Marekani
 Dar es Salaam
TANZANIA
25 Juni, 2020
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI




Tamko Kuelezea Masikitiko Yetu Kuhusu Uhuru wa Kujieleza na Ushiriki Jumuishi wa Kisiasa

Ubalozi
wa Marekani umesikitishwa na hatua za hivi karibuni za Serikali ya Tanzania za kuminya demokrasia, ikiwa ni pamoja na kuwakamata viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani wakiwa katika vikao vyao vya ndani na kufuta leseni ya gazeti la chama cha siasa cha upinzani. Hatua hizi ni mwendelezo wa mlolongo wa matukio ya kusikitisha ya vitisho kwa wanachama wa vyama vya upinzani, asasi za kiraia na vyombo vya habari. Haki ya kukusanyika kwa amani na uhuru wa kujieleza ni mambo yaliyojumuishwa na yanayolindwa na Katiba ya Tanzania na Tamko la Kimataifa la Haki za Binadamu. Ubalozi wa Marekani unafahari kusaidia na kuunga mkono uhuru wa kujieleza na ushiriki jumuishi wa kisiasa kwa namna zote.


Kwa maelezo zaidi, tafadhali wasiliana na Kitengo cha Habari cha Ubalozi wa Marekani Dar es Salaam kwa simu Na: +255 22 229-4000 au barua pepe: DPO@state.gov.




Statement of Concern about Freedom of Expression and Inclusive Political Participation

The Embassy of the United States of America expresses concern over recent actions by the Government of Tanzania to stifle democratic norms, including the arrest of political opposition figures during a closed party meeting and the revocation of the media license of an opposition party newspaper. These actions follow a disconcerting pattern of intimidation toward opposition members, civil society, and media outlets. The Rights to Peaceful Assembly and Freedom of Expression are enshrined in the Tanzanian Constitution, and in the Universal Declaration of Human Rights. The U.S. Embassy proudly supports freedom of expression and inclusive political participation in all formats.

By U.S. Embassy Dar es Salaam | 25 June, 2020


No comments :

Post a Comment