Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, October 5, 2013

Dk. Shein afanya mazungumzo kuimarisha uhusiano na Uingereza

NA MWANDISHI WETU

5th October 2013


Rais wa Zanzibar,Dk. Ali Mohamed Shein
Rais  wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Idara ya Afrika Mashariki na Magharibi katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Uingereza  Harriet Mathews kuhusu kuimarisha uhusiano na ushirikiano kati ya Zanzibar na Uingereza.

Katika mazungumzo hayo Dk Shein  ameishukuru Serikali ya Uingereza kwa misaada yake kwa Zanzibar na kueleza matumaini yake kuendeleza ushirikiano zaidi katika kusaidia Zanzibar kutimiza ndoto yake ya kuwa taifa lenye uchumi wa kipato cha kati ifikapo mwaka 2020.

Alimueleza Mathews kuwa uwekezaji ni sehemu muhimu ya kupanua ushirikiano kati ya Uingereza na Zanzibar na kutoa wito kwa wawekezaji wa nchi hiyo kuzitumia fursa za uwekezaji zilizopo nchini hasa katika sekta ya Utalii na Uvuvi wa Bahari Kuu.

Alisema pamoja na kuwepo fursa katika sekta nyingi za uchumi, sekta ya uvuvi wa bahari kuu ni eneo ambalo likipata uwekezaji muafaka lina kila uwezo wa kubadili maisha ya wananchi wengi wa Zanzibar.

Dk. Shein alieleza kuwa eneo hilo linagusa maisha ya wananchi wengi na anaamini kuwa linaweza kusaidia kufikia malengo ya Serikali sio tu ya kuinua kiwango cha ukuaji wa uchumi wa nchi bali hata kuinua kiwango cha maisha ya wananchi wa Zanzibar kwa kutoa ajira nyingi.

Kwa upande wake, Mathews alisema Uingereza itaendelea kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kutekeleza mipango yake ya maendeleo ili kunyanyua kiwango cha maisha cha wananchi wake.

Alisema Serikali ya nchi yake inaiona Zanzibar kuwa mshiriki muhimu katika mpango wa ushirikiano kati ya Uingereza na Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kusaidia kufikia malengo ya maendeleo.

“Zanzibar ni mshiriki muhimu katika Mpango wetu wa Ushirikiano kati ya Uingereza na Afrika Mashariki ili hatimae iweze kufikia lengo lake la kuingia katika nchi zenye uchumi wa kipato cha kati,” alisema Mathews.
 
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment