Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, October 4, 2013

Watanzania waaswa kununua hisa DSE

NA MWANDISHI WETU

4th October 2013


Mkurugenzi Mtendaji wa benki mpya ya Maendeleo, Ibrahim Mwangalaba
Watanzania wametakiwa kununua hisa zinazouzwa kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) kwa lengo la kumiliki sehemu ya kampuni zilizosajiliwa na kuongeza wigo wa uchumi na kukuza kipato.

Ushauri huo ulitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa benki mpya ya Maendeleo, Ibrahim Mwangalaba, wakati akielezea umuhimu wa hisa na maendeleo.

Alisema kwa kutambua umuhimu huo, benki hiyo inatarajia kusajili hisa zake DSE na kuwawezesha Watanzania kuzimiliki.

Benki yetu imesajiliwa katika soko la Hisa na Mitaji na hivyo kuwa ni benki ya kwanza nchini kuanza biashara na kusajiliwa moja kwa moja katika soko hilo.

Hivi sasa jumla ya hisa milioni nane zinauzwa katika soko la awali kwa bei ya Sh. 500 kwa hisa.

Alidokeza kuwa baada ya uuzaji wa hisa za Maendeleo Bank kufikia ukomo Oktoba 15, mwaka huu, Benki ya Maendeleo itatangazwa rasmi kuwa moja kati ya taasisi zitakazokuwa kwenye soko la DSE.
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment