Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, October 8, 2013

Wawili mbaroni kwa kuingia na bastola Z`bar

NA MWANDISHI WETU

8th October 2013


Kamishna wa Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa
Watu  wawili wamekamatwa na silaha katika bandari ya Zanzibar wakati wakitokea Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Mkadam Khamis Mkadam, alisema watu hao walikamatwa na bastola aina ya cz 92 ikiwa na risasi nane wakati wakitokea Dar es Salaam kwa boti ya Kilimanjaro 4.

Alisema baada ya wahatumiwa hao kuhojiwa walieleza kuwa ni wamiliki halali wa silaha hiyo, lakini Kamanda huyo alisisitiza kuwa sheria ya watu kumiliki silaha haitumiki  Zanzibar.

Alisema watu hao watafikishwa mahakamani. Aliwataja kuwa ni Daudi Obeto Matiku (40) na Emanual Joseph Obeto (35).

Hatua hiyo imekuja baada ya Kamishna wa Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa, kuvitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuimarisha ulinzi na usalama ili  kupambana na wahalifu.
 
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment