TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR
TAARIFA YA MWENYEKITI WA TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR
MHE. JECHA SALIM JECHA KWA VYOMBO VYA HABARI TAREHE
25 OKTOBA 2015
Ndugu Wananchi,
Kesho Jumapili tarehe 25 Oktoba 2015 ni siku ya Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar
ambapo wananchi wa Zanzibar watapiga kura kumchagua, Rais wa Zanzibar,
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Madiwani kwa upande mmoja na
kumchagua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wabunge kwa upande
mwengine.
Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar imekamilisha taratibu zote muhimu
zitakazowawezesha wapiga kura kupiga kura bila ya usumbufu. Aidha, vifaa
vyote muhimu vinavyohusika na kazi ya kupigisha kura vimepatikana na
vimeshasambazwa katika vituo vyote vya kupigia kura Unguja na Pemba.
Ndugu wananchi, uchaguzi ni zoezi ambalo hufanyika kwa misingi ya Sheria,
linalohitajia utulivu na usalama wa hali ya juu. Kwa hivyo, siku ya kupiga kura,
Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar inawaomba wananchi wote kuzingatia ipasavyo
maelekezo ambayo yametolewa na yatakayotolewa na Tume ya Uchaguzi katika
vituo vya kupigia kura, kwani maelekezo hayo yatatolewa kwa kufuata mwongozo
wa Sheria na yanalenga kudumisha utulivu wakati wote wa kupiga, kuhesabu na
kujumlisha kura katika vituo. Tume ya Uchaguzi inawasihi wapiga kura wote
kuwa endapo katika zoezi la upigaji kura kutajitokeza tatizo kwa upande wa vifaa
ni vyema wafuate taratibu za sheria katika kulitafutia ufumbuzi na kamwe
Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar inawaomba wananchi kuyafahamu na kuyaelewa
mambo yafuatayo kuwa:-
1. Upigaji kura utafanyika katika vituo vya kupigia kura ambavyo vitakuwa na
wastani wa wapiga kura 350. Kila kituo cha kupigia kura kitakuwa na
Msimamizi ambaye atakuwa ndiye kiongozi na mdhamini wa shughuli za
uchaguzi katika kituo husika. Pia, kutakuwa na Wasimamizi Wasaidizi wa kituo
ambao watafanya kazi chini ya dhamana ya Msimamizi wa kituo.
2. Kila mwananchi aliyejiandikisha kuwa mpiga kura kwa uchaguzi wa Zanzibar
na aliyekuwa na shahada ya kuandikishwa kuwa mpiga kura kwa Uchaguzi wa
Zanzibar, na ambaye taarifa zake zitakuwemo katika Daftari la wapiga kura
atakuwa na haki ya kupiga kura kumchagua Rais wa Zanzibar, Mjumbe wa
Baraza la Wawakilishi na Diwani kwa upande mmoja na kwa upande
mwengine atapiga kura kumchagua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
3. Upigaji kura utafanyika katika eneo ambalo mtu amejiandikisha au karibu na
sehemu hiyo. Katika kila kituo cha kupigia kura kutakuwa na watendaji wa
Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar na Tume ya Taifa ya Uchaguzi pamoja na
maandishi yanayowaelekeza wapiga kura kujua wapi watapiga kura kwa ajili
ya kumchagua Rais wa Zanzibar, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na
Diwani kwa uchaguzi wa ZEC na Rais wa Jamhuri ya Muungano na Mbunge
kwa upande wa NEC. Aidha, katika kila kituo cha kupigia kura, kutakuwa na
mawakala wa vyama vya siasa ambao watakuwa na jukumu la kuwakilisha na
kulinda maslahi ya wagombea wa vyama vyao katika kituo, kugundua watu
wanaojifananiza (personation) na kushirikiana na Msimamizi wa kituo na
Wasimamizi Wasaidizi wa vituo juu ya usimamizi mzuri wa sheria katika kituo.
4. Kuwa vituo vyote vya kupigia kura vitafunguliwa saa 1.00 asubuhi na
kufungwa saa 10.00 jioni. Muda huo utakapomalizika hakuna mpiga kura
atakayeruhusiwa kujiunga katika msitari wa kuingia katika kituo cha kupigia
kura, bali watakaokuwa katika misitari ya kuingia kituoni ndani ya muda huo,
wataendelea na upigaji kura hadi mtu wa mwisho atakapomalizika. Itakapofika
saa 10 kamili askari atasimama nyuma ya mtu wa mwisho katika mstari. Mtu
yeyote atayekuja baada ya hapo hataweza kupiga kura.
5. Kila mpiga kura ajitahidi kufika mapema katika kituo cha kupigia kura na
ahakikishe kuwa amechukuwa shahada yake ya kupigia kura. Na kuwa, iwapo
atawakuta watu wengine wamejipanga katika mstari, ajipange nyuma yao bila
ya usumbufu.
6. Wapiga kura wagonjwa na ambao hawawezi kupiga kura wenyewe,
wanaruhusiwa kwa mujibu wa Sheria kwenda vituoni na watu wanaowaamini
ili kuwasaidia kupiga kura. Hairuhusiwi na ni marufuku kwa mtu asiyekuwa na
sifa za kupigiwa kura kupigiwa kura. Endapo itabainika Mkuu wa Kituo cha
kupigia kura au Msaidizi wake ataruhusu mtu au watu wasiostahiki kupigiwa
kura hatua za kinidhamu na sheria zitachukuliwa mara moja. Tume inawasihi
Wakuu wa Vituo na Wasaidizi wao kuwa waangalifu sana na makosa hayo.
7. Hairuhusiwi kuendesha kampeni ya aina yoyote katika vituo vya kupigia kura.
Na kuwa, si ruhusa kwa mpiga kura au wapiga kura kuvaa sare au alama za
vyama vyao vya siasa au wagombea wanapokwenda kupiga kura. Aidha, ni
marufuku kwa wapiga kura kwenda katika vituo vya kupigia kura wakiwa
wamebeba silaha za aina yoyote kwa njia ya dhahiri au kificho.
8. Mtu yeyote haruhusiwi kubaki kituoni baada ya kupiga kura yake. Hivyo, Tume
ya Uchaguzi ya Zanzibar inawasihi wapiga kura mara wanapomaliza kupiga
kura waondoke vituoni na kurejea nyumbani au kwenda katika shughuli zao
nyengine. Inasisitizwa mzunguuko wa mita mia mbili kutoka kituo cha kupigia
kura hapatakiwi kuonekana mtu yeyote asiyestahiki.
9. Kila mgombea anaruhusiwa kuweka wakala mmoja katika kituo cha kuhesabia
kura na kujumlishia kura. Kila wakala wa mgombea atapatiwa nakala ya fomu
ya matokeo ya hesabu ya kura kituoni baada ya kura kuhesabiwa katika kituo na
nakala ya fomu ya matokeo ya jimbo au wadi baada ya kura kujumlishwa.
10.Hakuna mtu mwengine yeyote zaidi ya watu waliotajwa katika Sheria ya
Uchaguzi anayeruhusiwa kuwepo katika eneo la kuhesabia kura. Aidha, hakuna
mtu zaidi ya waliotajwa katika sheria atakayeruhusiwa kuwepo katika masafa
ya mita mia mbili kutoka pahala panapohesabiwa kura.
11.Kazi ya kujumlisha na kuhesabu kura kwa wagombea Uwakilishi na Udiwani
kwa vituo itafanywa katika vituo maalum katika kila jimbo. Katika vituo hivyo,
wagombea wote watakaoshinda kwenye chaguzi hizo (Uwakilishi na Udiwani)
ndimo watakamotangazwa na Wasimamizi wa Uchaguzi wa majimbo husika.
12.Kazi za kujumulisha hesabu za kura kwa wagombea Urais wa Zanzibar
zinafanywa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kwa mujibu wa Sheria, na ni
Tume ya Uchaguzi peke yake ndiyo yenye madaraka ya kumtangaza mshindi
wa kiti cha Urais wa Zanzibar baada ya kuthibitisha matokeo ya mshindi.
13.Ni makosa kufanya mambo yafuatayo wakati wa zoezi la upigaji wa kura:-
Kutaka kupiga kura kabla ya kituo hakijafunguliwa au baada ya kufungwa.
Kupiga kura au kukusudia kupiga kura kama huna haki ya kufanya hivyo.
Kupiga kura au kukusudia kupiga kura zaidi ya mara moja katika uchaguzi
mmoja.
Kupiga kura kwa jina la mtu mwengine, aliyehai, aliyekufa au kwa njia ya
udanganyifu.
Kutia ndani ya sanduku la kura kitu chengine chochote zaidi ya kura.
Kuingiza au kuharibu karatasi ya kura au shahada ya matokeo au fomu
yoyote inayohusiana na uchaguzi.
Kujaribu kumshawishi mpiga kura kumchagua mgombea maalum.
Kutaka kujua mgombea ambaye mpiga kura anakusudia kumpigia kura au
aliyempigia kura.
Ndugu Wananchi na Viongozi wa Vyama vya Siasa cha muhimu kuliko yote
katika maelezo yangu ni matokeo baada ya zoezi la kupiga na kuhesabiwa kwa
Katika hilo naomba kuwakumbusha kuwa katika ushindani wowote ule kuna
kushinda na kushindwa. Hivyo, ni vyema kwa wagombea na wafuasi wa
wagombea na vyama vyao kuwa tayari kwa matokeo ya ama kushinda au
kushindwa. Na pale ambapo mgombea hakuridhika na matokeo ni vyema akatumia
njia au taratibu za kisheria katika kutoa malalamiko yake. Njia nyengine yoyote
mbadala wa hiyo wakati wa kushughulikia maalamiko ya kiuchaguzi inaweza
kuondoa utulivu na kupelekea hasara kubwa kwa nchi yetu.
Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kwa upande wake inafanya kila linalowezekana
katika kuendesha Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wa tarehe25 Oktoba 2015 kwa
salama na amani na pia itahakikisha kuwa Uchaguzi mwaka 2015 unakuwa huru
na wa haki.
14. Ndugu wananchi imebainika tabia kwa baadhi ya wafuasi wa vyama vya
Siasa kuwa siku ya kupiga kura au kabla ya hapo kuwanyanganya vitambulisho
vya kupigia kura wapiga kura wa Chama au vyama vyengine au kuvinunua kwa
madhumuni ya kuwazuia kupiga kura na eti kupunguza kura za vyama
vyengine, mara nyengine huwatisha au kuwasusia huduma za kijamii. Hayo ni
makosa yasiyovumilika. Tume ina waonya watu wote wenye tabia ya aina hiyo
waache mara moja. Atayebainika na vitendo hivyo atachukuliwa hatua za
kisheria. Mpiga kura yeyote atayepatwa na kadhia ya aina hizo atoe taarifa
kwenye mamlaka zinazohusika kama vile Tume yenyewe au Polisi. Vyama vya
siasa vinaombwa kuwatahadharisha wafuasi wao kutojingiza katika makosa ya
aina hiyo.
Nawatakia wananchi wote wa Zanzibar kila kheri na mafanikio katika upigaji wa
kura kesho tarehe 25 Oktoba, 2015.
Ahsanteni kwa kunisikiliza.
JECHA SALIM JECHA
MWENYEKITI,
TUME YA UCHAGUZI
No comments :
Post a Comment