AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, December 10, 2015

Ofisa afya mbaroni kwa uchafu

Chiku Gallawa. 
By Waandishi Wetu, Mwananchi
Musoma. Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Zelothe Stephen ameamuru kutiwa mbaroni Ofisa Afya wa Kata ya Mkendo, Desideri Rwegoshora kwa kushindwa kusimamia usafi katika maeneo ya kata yake.
Zelothe alitoa amri hiyo  baada ya kufanya ukaguzi katika kata zote na kubaini  mazingira ya kata  hiyo yamekithiri kwa uchafu na kukaidi maagizo aliyotoa katika kamati ya usafi ya wilaya.
 Alisema katika kata hiyo kuna soko kuu la wilaya linalotegemewa na wakazi wengi wa Musoma, lakini limekithiri kwa uchafu.
Dodoma
Naye  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Chiku Gallawa akizungumza wakati wa kufanya usafi katika soko la Chang’ombe, amepiga marufuku uuzaji wa mifuko ya rambo na kuwaagiza watendaji kukagua mifuko hiyo katika maduka.
Handeni
Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Husna Msangi amewataka wafanyabiashara wa kwenye masoko na migahawani kuzingatia kanuni za usafi na kuacha tabia ya kulalamika kuwa Serikali inawanyanyasa.

No comments :

Post a Comment