zanglassworks

AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, January 31, 2016

ROBERT MUGABE TALKS AT THE 26TH AFRICAN UNION SUMMIT!


THE ONCE POWERFUL ZENJ EMPIRE!


Siku nne shubiri kwa Serikali bungeni

By Fidelis Butahe
Dodoma. Zilikuwa siku nne ngumu kwa Serikali bungeni. Ndivyo unavyoweza kuelezea hali ilivyokuwa kwenye chombo hicho cha kutunga sheria katika siku za mwanzo za mkutano wa pili wa Bunge la Kumi na Moja.
Mkutano huo ulioanza Jumanne, ulikumbwa na mlolongo wa maombi ya mwongozo kuhusu uamuzi wa kituo cha televisheni cha Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) kupunguza matangazo ya moja kwa moja ya shughuli za Bunge.
Jumanne ilikuwa siku ya kujadili hotuba ya Rais John Magufuli, na siku ya pili tu wabunge wa upinzani walihoji uamuzi wa TBC kupunguza matangazo ya moja kwa moja, wakiwasema unawanyima wananchi haki ya kikatiba ya kupata habari.
Jumatano mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko aliuliza swali kuhusu elimu bure na baada ya majibu, wabunge wengi walisimama kutaka kuomba mwongozo na waliponyimwa walipiga kelele zilizosababisha mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge kuita polisi ili wawaondoe wabunge wa upinzani kwa nguvu.

BOARD YA ZACADIA YAKUTANA TORONTO KUPANGA MIKAKATI YA 2016!

WANA-BOARD WA ZACADIA WAKIONEKANA KWENYE MKUTANO WAO WA TAREHE 30 JANUARY, 2016 ULIOFANYIKA NORTH YORK (TORONTO) WAKIPANGA MIKAKATI YA 2016.




Why children must learn about money

  • Like most things, it's good to learn about money and, most importantly, to start implementing the learnings at a young age.
Good financial skills are vital to ensure, as adults, we get through life without too many bumps or pitfalls. From making a savings plan to ensure security after retirement or in the case of an emergency, to avoiding debt, a healthy understanding of the concept of money is essential.

Like most things, it's good to learn about money and, most importantly, to start implementing the learnings at a young age.

However, still today many children grow up into adults who can't properly save, spend and budget. In fact, a recent survey on savings carried out by compareit4me.com on UAE residents highlighted this. 

Our findings revealed that 53 per cent of respondents don't think they earn enough to allow them to put anything into savings, with over 30 per cent admitting they do not save a single dirham and 13 per cent say they believe life is too short to save. 

These are quite worrying statistics, especially given the fact pensions and social benefits don't exist in the UAE, so even greater importance should be given to financial goals.

To avoid the next generation making bad financial decisions and to help them enjoy financially fit lives, children need to be taught the essentials about money.

Man murders wife over marital dispute in Sharjah


The suspect allegedly stabbed his wife in various parts of her body at their apartment which they shared with other family in Abu Shagara.

Sharjah Police on Saturday arrested a 42-year-old Pakistani man for allegedly murdering his wife due to marital disputes.

The suspect identified as M.K allegedly stabbed his wife in various parts of her body at their apartment which they shared with other family in Abu Shagara.

Police said that they received a call at the operation room about the incident and dispatched a police team comprising forensic experts, CID officers, patrols and ambulance who reached the site and found the body of the woman in a pool of blood.

They also found that the suspect was detained by the people who shared the apartment when he tried to flee the scene after he committed the murder.

One of the witnesses who lived in the same apartment told the police that he heard the fight between the couple and he knocked the door but no one opened.

Let Seawings plan your next exciting getaway

Get a breathtaking view of Dubai onboard Seawings.

Dubai is no short of activities with many options to make the best of the cool weather and ensure fun for the entire family. Adding to the list of things to do, Seawings, a luxury seaplane tour operator, recently launched a holiday package that combines seaplane excursions with exceptional hospitality experiences at leading luxury hotels and resorts within the UAE and Oman.

Accommodation options in the UAE include signature properties and brands such as Anantara, Bab Al Shams, Le Royal Meridien, Park Hyatt, Banyan Tree, Six Senses and Al Maha Desert Resort & Spa.

The seaplane experience includes luxury seating and an exciting water takeoff and landing onboard a spacious Cessna Caravan Amphibian Seaplane. Additionally, every seat is a window seat, offering unparalleled views of the UAE and Oman's natural and man-made iconic landmarks.

Those interested can book their plans via the Seawings Lifestyle website. Visitors can look for packages online or get in touch with the Seawings team for assistance. Each getaway can be customised to suit individual requirements.


For more information, visit www.seawingslifestyle.com

FUONI PETROL STATION KUANZA KAZI WIKI ZA MWANZO ZA FEBRUARY, 2016 BAADA YA KUJENGWA UPYA!


Ngeze: Rais Magufuli apewe uenyekiti CCM ili aisafishe

Kada wa CCM, Pius Ngeze, akifafanua jambo wakati akihojiwa na gazeti hili mkoani Kagera hivi karibuni. Picha na Phinias Bashaya
By Phinias Bashaya, Mwananchi
Ingawa kwa baadhi ya watu siasa ni mchezo mchafu, kwa Pius Ngeze (73), kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM )aliyeshiriki kwenye harakati za siasa za serikali za awamu zote tano, hali ni tofauti.
Ngeze, ambaye amewahi kuwa mbunge wa Ngara kuanzia mwaka 1995 hadi mwaka 2000 kwa tiketi ya CCM, anasema siasa ni nzuri ikimpata kiongozi sahihi. Akizungumza katika mahojiano maalumu na gazeti hili mkoani Kagera hivi karibuni, kada huyo mkongwe ametaka Rais John Magufuli akabidhiwe uenyekiti wa CCM ili akisafishe na kukisuka upya chama hicho.
Ngeze anasema wakati Rais Magufuli akiendelea ‘kutumbua majipu’ kwenye sekta na idara za umma, akumbuke kuwa hata ndani ya CCM yapo majipu yanayohitaji kupasuliwa ili kukiboresha zaidi chama hicho.
Kwa utaratibu wa CCM, Rais hukabidhiwa uenyekiti wa chama hicho katika uchaguzi unaofanyika baada kuingi Ikulu, ingawa katika miaka ya karibuni Rais anayeondoka madarakani huachia mapema uenyekiti.

TUJIKUMBUSHE: IS MAGUFULI THE REAL DEAL!


Polisi yakataa kusafirisha mwili wa askari jambazi

Kamanda wa polisi mkoa Katavi, Dhahiri Kidavashari.
By Mussa Mwangoka
Katavi. Jeshi la Polisi mkoani Katavi limegoma kuusafirisha mwili wa askari Nobert Chacha (25) aliyeuawa kwa kupigwa risasi kifuani katika tukio la ujambazi nyumbani kwa mfanyabiashara wa madini.
Habari zilizopatikana kutoka mjini Mpanda zinasema mwili wa marehemu ulisafirishwa jana kwenda mkoani Mara na baadhi ya marafiki zake walioshirikiana na Chama cha Wenyeji wa Mara waishio mkoani Katavi.
Mjumbe wa chama hicho, Julius Marwa alisema walilazimika kusafirisha mwili huo baada ya Polisi kukataa kuusafirisha kwa madai kuwa kitendo alichofanya askari huyo tayari alikuwa amejifukuzisha kazi.
Kamanda wa polisi mkoani humo, Dhahiri Kidavashari alisema kwa taratibu za jeshi, mwili huo haukustahili kupewa heshima yoyote, ikiwa ni pamoja na kusafirishwa kwa kuwa ni aibu na fedheha kutokana na kitendo alichofanya.

Al Jazeera English HD Live Stream!


SERIKALI YATOA VIPAUMBELE VYAKE KWA WANANCHI

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dkt. Servacius Likwelile (katikati) akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es salaam kuhusu Serikali ilivyojipanga kuboresha na kuhudumia sekta mbalimbali nchini ikiwemo elimu, umeme, maji na miundombinu. Kulia ni Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Alfayo Kidata na kushoto ni Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Prof. Benno Ndulu.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Prof. Benno Ndulu akisistiza wakati wa mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es salaam kuhusu mapato na matumizi ya Serikali yalivyoboreshwa na uchumi wa nchi kuimarika na kutengemaa. 

Serikali imetoa jumla ya Sh. Bilioni 318.406 kwa mwezi wa Januari mwaka 2016, kwa ajili ya miradi ya maendeleo nchini na Sh. Bilioni 538.5 kwa mishahara ya watumishi wa Umma.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Servacius Likwelile alisema kuwa Serikali inajivunia kufanikiwa kutumia fedha za ndani kwa ajili ya miradi ya maendeleo ambapo hadi sasa Serikali imetumia kiasi cha Sh. Bilioni 71.2 tu kutoka fedha za nje.

Dkt. Likwelile alisema mapato yanayokusanywa nchini yamewezesha kutekeleza sera ya elimu bure ambapo mwezi Desemba mwaka 2015 Serikali ilitoa kiasi cha Sh. Bilioni 18.77 kwa shule za msingi na sekondari kwa ajili ya ruzuku, ada na chakula kwa shule za bweni pamoja na mahitaji mengine ambapo mwezi wa Januari 2016 Serikali imetoa kiasi cha Sh. Bilioni 18.77 kwa ajili ya kutekeleza Sera hiyo.

Aliongeza kuwa katika ulipaji wa madeni ya wakandarasi nchini , Serikali imetoa Sh. Bilioni 130 kwa mwezi Januari mwaka 2016 ambapo mwezi Desemba mwaka 2015 ilitoa Sh. Bilioni 193.

RAIS MAGUFULI AWAAPISHA MNADHIMU MKUU WA JWTZ, BALOZI WA TANZANIA KUWAIT NA KATIBU TAWALA WA KATAVI NA MWANZA IKULU DAR ES SALAAM

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimuapisha Dkt. Mahadhi Juma Maalim kuwa Balozi wa Tanzania  Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimuapisha  Luteni Jenerali Venance Salvatory  Mabeyo  kuwa Mnadhimu Mkuu wa JWTZ  Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimuapisha Kamishna wa Polisi Clodwig Mathew Mtweve  kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza  Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimuapisha Kamishna wa Polisi Paul Amani Moses Chagonja kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  na viongozi wa Jeshi la Wananchi na Jeshi la Polisi  katika picha ya pamoja baada ya kuapishwa Mnadimu Mkuu wa TPDF, Balozi wa Tanzania Kuwait na  Katibu Tawala wa Mikoa ya Katavi na Mwanza Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016

MAJANGILI YATUNGUA HELIKOPTA, YAUA RUBANI WA RANCHI YA WANYAMAPORI MEATU

 Kwa mara ya kwanza katika historia ya uhifadhi nchini Majangili wamempiga risasi na kumuua Rubani Roger na kuangusha helikopta aliyokuwa akitumia kwa risasi. Alikuwa akienda kuongeza nguvu ya askari wa uhifadhi waliokuwa wakipambana na majangili hatari wilayani Meatu, Simiyu katika ranchi ya wanyamapori ya Mwiba.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe akiangalia Helikopta iliyolipuliwa na majangili alipotembelea eneo la tukio.

Damu kwenye kiti

TANZANIA MAGAZETINI LEO!



WAZIRI MKUU MAJALIWA AONGOZA MBIO ZA HAPA KAZI TU DODOMA HALF MARATHON

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongoza mbio za Wabunge za Hapa Kazi Tu Dodoma Half Marathon zilizoanzia Bungeni hadi uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Januari 30, 2016. Kushoyo kwake ni Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye na kushoto ni Naibu Spika wa Bunge, Dkt Tulia Ackson. Mwansasu (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Baadhi ya Washiriki wa mbio za Hapa Kazi Tu Dodoma Half Marathon wakishiriki mbio hizo mjini Dodoma Januari 30, 2016.
Mmoja wa wapigapicha walioshiriki mbio za Hapa Kazi Tu Dodoma Half Marathon alilazimika kuomba msaada kwa askari wa usalama barabarani Mjini Dodoma Januari 30, 2016. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi ufunguo wa pikipiki mshindi wa kwanza wa mbio za Hapa Kazi Tu Dodoma Half Marathon upande wa wanaume, Emmanuel Giriki kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Januari 30, 2016.

Balozi Amina: Bado nautaka urais

Balozi Amina Salum Ali .

By Kizitto Noya
Amina Salum Ali, ambaye alishika nafasi ya pili kwenye mbio za urais ndani ya CCM, amesema ndoto yake ya kushika nafasi hiyo ya juu katika siasa nchini, haijafa.
Amina, ambaye alikuwa balozi wa Afrika kwenye Umoja wa Mataifa, alisema hayo kwenye mahojiano maalum na Mwananchi yaliyofanyika mapema wiki iliyopita jijini Dar es Salaam.
Balozi Amina alichomoza kwenye mbio za urais ndani ya CCM baada ya kuingia tano bora, akiwa pamoja na John Magufuli, Asha Rose Migiro, January Makamba na Bernard Membe na baadaye kuingia tatu bora kwa ajili ya kupigiwa kura na Mkutano Mkuu wa chama hicho ambao ulimchagua Magufuli kugombea urais.
Lakini Balozi Amina, ambaye hivi sasa ana umri wa miaka 59, anasema hilo halijaondoa ndoto yake ya kuingia Ikulu.
“Sikushiriki Uchaguzi Mkuu mwaka jana kwa ajili ya kujaribu bahati yangu, bali nilikuwa na nia ya dhati ya kushinda urais na kuwatumikia wananchi,” alisema Balozi Amina.

Mikarafuu yaungua bonde la Mkanyageni, Pemba

Image result for mashamba ya karafuu zanzibar


Image result for mashamba ya karafuu zanzibar
Na Masanja Mabula –Pemba 
Zaidi ya mikarafuu 151 umeungua katika tukio la moto lililotokea Janauri 22 mwaka huu katika bonde la Mkanyageni Shehia ya Mzambarauni Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba .

Jumla ya eka tisa (9) za mashamba ya mikarafuu yameathiriwa zimehujumiwa kwa kuchomwa moto na watu wasiojulikana na kusababisha hasara kuwa kwa wamiliki ya mashamba hayo .

Akizungumza katika eneo la tukio Mkuu wa Wilaya ya Wete Rashid Khadidi Rashid amevitaka vyombo vya ulinzi kufanya uchunguzi wa kina ili kuwabaini waliohusika wa kitendo hicho .

Amesema kuwa kitendo cha kuchoma moto mashamba hayo ni kuhujumu uchumi wa nchi pamoja na wananchi wake na kwamba serikali itahakikisha wanahusika wanakamatwa na kufikishwa mahakamani.

HAPPY BIRTHDAY VIJIMAMBO!

LEO NI HEPI BESDEI YA BLOG YA VIJIMAMBO YATIMIZA MIAKA 6


 Vijimambo ilizaliwa Januari 31, 2010 na kuzinduliwa Oktoba 23, 2010 na aliyekua Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Mwanaidi Maajar. Picha ni siku ya uzinduzi ukumbi wa Mirage  uliopo Hyattsville, Maryalnd.
Hapa Balozi Mwanaidi Maajar akiwa mgeni rasmi miaka 2 ya Vijimambo iliyofanyika Machi 31, 2012 ukumbi wa Mirage uliopo Hyattsville, Maryalnd.
 
Rais mstaafu Mhe. Ali Hassan Mwinyi akiwa mgeni rasmi kwenye sherehe ya miaka 3 ya Vijimambo iliyofanyia Julai 6, 2013 katika ukumbi wa Hampton Inn uliopo Capitol Heights. Maryland.
Mwenyekiti wa Vijimambo akiwapokea wasanii Shilole na Masanja waliokuja kunogesha sherehe ya miaka 3 ya vijimambo.
Mhe. Nyarandu (kulia) akiwa mgeni rasmi kwenye sherehe ya miaka 4 ya Vijimambo iliyofanyika Septemba 13, 2016 Hotel ya Growne Plaza iliyopo Rockville, Maryland.

CCM Imeridhika na maamuzi ya Tume ya Uchaguzi, Zanzibar

Image result for ccm of tanzania


CHAMA
cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimeelezea kuridhishwa kwake na maamamuzi ya Tume ya uchaguzi Zanzibar (ZEC) kwa kutangaza siku ya kufanyika kwa uchaguzi wa marudio kwa nafasi ya Urais, Uwakilishi na Udiwani.

Kimesema kuwa maamuzi hayo ya kufanyika uchaguzi huo Machi 20 mwaka huu, yanaenda sambamba na matakwa ya wananchi waliokuwa wengi katika kutekeleza haki yao ya kidemokrasia kwa mujibu wa miongozo ya katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar, Waride Bakar Jabu alisema kwamba CCM inaungana na vyama vingine vya kisiasa nchini vilivyobaini kasoro za uchaguzi mkuu uliopita kuwa na kasoro kwa kuunga mkono maamuzi ya ZEC kuwa ni sahihi kwani yamefuata hatua muhimu za Kikatiba.

Waride alisema msimamo wa CCM katika Mkwamo wa kisiasa uliopo Zanzibar ni kurudi katika uchaguzi wa marudio ili kila chama cha kisiasa kinachoshiriki katika uchaguzi uliopita kiweze kupata haki ya kungia madarakani kwa njia za halali na zinazokubalika kisheria.

Rais apanga safu JWTZ


Mkuu wa Majeshi, Jenerali Devis Mwamunyange akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana. Picha na Said Khamis

By Elizabeth Edward
Dar es Salaam. Rais John Magufuli ameendelea kupanga safu za taasisi za Serikali baada ya kufanya uteuzi wa maofisa mbalimbali wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ), huku akimuongezea muda Mkuu wa Majeshi, Jenerali Davis Mwamunyange.
Akitangaza mabadiliko hayo, Jenerali Mwamunyange, ambaye ameongezewa mwaka mmoja, alisema uteuzi huo umefanywa kuziba nafasi za maofisa waliostaafu kwa mujibu wa sheria, na walioteuliwa kushika nafasi mbalimbali za uongozi serikalini.
Mwamunyange, ambaye alitakiwa kustaafu leo Januari 31 sambamba na maofisa wengine, ataendelea kulitumikia jeshi hilo mpaka Januari 31 mwakani.
Aliwataja walioteliwa kuwa ni Luteni Jenerali Venance Mabeyo anayekuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi nafasi iliyoachwa wazi na Luteni Jenereali Samwel Ndomba aliyemaliza muda wake wa utumishi.

Panga la JPM lachinja vichwa 152

Rais John Magufuli.
By Florence Majani na Suzan Mwillo
Dar es Salaam. Hakuna shaka kuwa Rais John Magufuli anatimiza ahadi yake ya kutumbua majipu aliyoitoa katika hotuba yake ya kwanza bungeni baada ya zaidi ya watumishi 152 wa Serikali kutimuliwa hata kabla ya siku 100 kutimia.
Hao ni watumishi waliotimuliwa kwa majina au vyeo vyao, lakini ukijumlisha na wengine waliosimamishwa au kufukuzwa kwa matamko bila kutajwa majina, idadi ni kubwa zaidi.
Watumishi hao wamesimamishwa na baadhi wamefukuzwa kazi kutokana na tuhuma mbalimbali za kukiuka Sheria ya Ununuzi wa Umma, Rais kutoridhishwa na utendaji wao, wizi kwenye taasisi zao, ukwepaji kodi, tuhuma za ubadhirifu wa fedha za umma na utovu wa nidhamu.
Hatua hizo ni utekelezaji wa ahadi ambazo Rais Magufuli alitoa kwenye hotuba yake ya kwanza bungeni Novemba 2, mwaka jana mjini Dodoma, alipoahidi kupambana na rushwa bila kigugumizi wala haya yoyote.

Halmashauri yasalimu amri kwa madiwani wa Ukawa

Halmashauri ya Jiji la Tanga imesalimu amri  kwa madiwani wa Ukawa waliokuwa wakipinga  uundwaji wa kamati za baraza hilo kwamba zimeundwa kinyemela ambapo Kaimu Mkurugenzi  amekubali kusitisha chaguzi za wenyeviti  wa kamati  hadi hapo taratibu zitakapo kamilika.

Halmashauri hiyo iliunda kamati za baraza hilo ambazo madiwani wa Ukawa walizikataa wakidai zimeundwa kinyume na sheria ya TAMISEMI na kulazimika kuunda tume ya kutaka ufafanuzi kwa Mkurugenzi  huyo kwa kuwa hana mamlaka ya kufanya hivyo.

Uchunguzi uliyofanywa na Nipashe ulibaini kuwa siku moja baada ya kaimu mkurugenzi huyo, Dk Wedson Sichalwe  kukutana na tume hiyo na kufanya mazungumzo nayo aliandika barua kwa wajumbe kusitisha zoezi la
uchaguzi wa wenyeviti wa kamati hizo.


Matapeli watumia jina la Jenerali Mboma

Matapeli wa mtandaoni wameingilia barua pepe ya Mkuu wa Majeshi mstaafu, Jenerali Robert Mboma na kuomba msaada wa Dola za Marekani 2,550 kwa watu zaidi ya 1,000.

Watu hao ambao bado hawajafahamika waliingia barua pepe ya Mboma Alhamisi na kutuma ujumbe kwa watu 1001, wakiwamo watu mashuhuri, wakiomba msaada huo.

Akizungumza na Nipashe Jumapili, Jenerali Mboma alisema katika tukio hilo ambalo limemshtua, watu hao baada ya kuingilia barua pepe hiyo walianza kutuma maombi ya msaada kwa watu ambao wapo katika barua pepe ambayo amekuwa akiitumia kwa mawasiliano na watu wake.

Alisema katika ujumbe huo ambao umeandikwa kwa lugha ya kiingereza, matapeli hao wameeleza kuwa Mboma amekwama katika mji wa Odesa, nchini Ukraine ambako alikwenda kwa mapumziko akiwa na familia yake.


SAVE THE CHILDREN ORGANIZATION HELPING ZANZIBAR'S WOMEN & KIDS!

Mwakilishi wa Shirika la Kimataifa la kupigania haki za watoto (Save The Children), Mali Nilsson (kulia), akikabidhi Bajaji mbili kwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Uwezeshaji,Ustawi wa Jamii, wanawake na watoto Msham Khamis (wa pili kushoto), zitakazotumika kukabiliana na vitendo vya unyanyasaji wanawake na watoto katika hafla iliyofanyika mjini Unguja, Zanzibar jana. (Picha: Mwinyi Sadallah)

Lowassa anavyoishi kama Rais nje ya Ikulu

Edward Lowassa
Licha ya kutotangazwa mshindi wa urais katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana, aliyekuwa mgombea wa nafasi hiyo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa, amekuwa na ratiba zinazofanana kwa kiasi fulani na Rais John Magufuli, imefahamika.

Kwa mujibu wa matangazo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Lowassa aliyekuwa akichuana kwa karibu na Magufuli katika muda wote wa kampeni za miezi miwili zilizoanza Agosti 21, 2015, alishika nafasi ya pili baada ya kupata asilimia 39.97 ya kura zote halali zilizopigwa.

Magufuli aliibuka mshindi baada ya kupata asilimia 58.46 ya kura hizo na aliapishwa Novemba 5, 2015 kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na tangu wakati huo ameendelea kusimamia mabadiliko kadhaa katika serikali yake ya awamu ya tano. 

Hata hivyo, Nipashe imebaini kuwa licha ya Lowassa kutotangazwa mshindi na kuingia Ikulu, mgombea huyo wa urais wa mwaka jana amekuwa na mwenendo wa matukio yanayofanana kwa kiasi kikubwa na ya kiongozi dola.

Lowassa alipinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu akidai alipokwa ushindi na NEC kwavile takwimu zake zinaonyesha alipata asilimia 60 ya kura zote halali.


How Dar hotel acquired extension plot illegally

Image result for bomoabomoa


Kinondoni Municipal Council in Dar es Salaam issued a title deed and a building permit illegally to Indian Ocean Hotel Limited for construction of an extension to its hotel at Masaki in the city, The Guardian on Sunday can report.

The dubious circumstances in which the two documents were issued to the company were laid bare yesterday after the ministry of Lands, Housing and Human Settlements Development, in collaboration with council officials, conducted a demolition of a temporary fence and other structures built in an open space along the edge of Golden Tulip Hotel premises in Masaki area.

It was earlier discovered that the plot in question had previously been temporarily leased by the municipal council to Indian Ocean Hotel Ltd, which operates Dar es Salaam Golden Tulip Hotel, for a parking lot during a Southern African Development Community (SADC) meeting last year.