dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Monday, December 5, 2016

Dkt.Shein acharuka, afanya ziara ya kushtukiza mkoa wa kaskazini unguja na kutoa miezi mitatu wizara ijenge kituo cha afya!

Katika hali isiyo ya kawaida Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapunduzi Dkt. Ali Mohamed Shein amefanya ziara ya kushtukiza katika mkoa wa kaskazini unguja na kutembelea kijiji cha wakaazi 200 ambacho kina ukosefu mkubwa wa huduma za kijamii huku akitoa miezi mitatu kwa wizara ya afya kujenga kituo cha afya daraja la kwanza.

Dkt. Shein alifika kijiii hicho cha mgonjoni kiwengwa mkoa huo wa kaskazini ambapo wakaazi hao wamekuwa hawana shule wala hudumaza afya,maji na umeme na kukuta ujenzi washule ya madarasa manne ujenzi wake ukiendelea ikiwa ni juhudi za wizara ya elimu  ambao viongozi wake walifika huko na kuona hakuna shule, Dkt. Shein amewahakikshia wakazi hao kuwa serikali iko kwa ajili yawanchi na amezitzka  wizara nyengine kuiga mfano huo wizara ya elimu ya viongozi kufika kwa wananchi na sio kukaa maofisni.

Kutokana na kujione hali hiyo Dkt. Shein ametoa miezi mitatu kwa wizara ya afya inajenga kituo  cha afya daraja la kwanza huku pia akizitaka  taasisi za mamlaka ya maji na umeme kuhakikisha katika kipindi hicho wanhahakikisha huduma zao zinafika eneo hilo kwa vile wananchi hao wanasathili huduma hizo.

No comments :

Post a Comment