Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, November 26, 2019

Rufaa kesi ya Abdul Nondo kusikilizwa kesho!

Rufaa ya kesi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP) Abdul Omari Nondo, inatarajiwa kusikilizwa kesho katika Mahakama Kuu kanda ya Iringa.

Katika rufaa hiyo, Nondo anawakilishwa na Mawakili watatu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania ambao ni Wakili Jebra Kambole, Chance Luoga na Shilinde Swedy.
Itakumbukwa kwamba Nondo alishtakiwa mwaka 2018 mwezi Machi kwa kutoa taarifa za uongo kinyume na Kifungu cha 16 cha Sheria ya Makosa Mtandaoni, ya mwaka 2015.

Hata hivyo, mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa ilitoa maamuzi na kumpa ushindi Nondo kwa kuwa upande wa mashtaka ulishindwa kuthibitisha mashtaka yao pasipo shaka. Baada ya kushindwa katika mahakama hiyo, upande wa Jamhuri walikata rufaa mahakama kuu kanda ya Iringa na usikilizwaji wa rufaa hiyo umepangwa kesho mbele ya Mhe. Jaji Penterine Kente.

No comments :

Post a Comment