dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, October 23, 2012

Dk Shein awaapisha makatibu wakuu leo

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi 
Dk. Ali Mohamed Shein,akimuapisha Dk.Juma Malik Akili, 
kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano,
katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar leo.

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,
akimuapisha Nd,Ali Khalil Mirza, kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi,Makaazi,
Maji na Nishati,katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar leo

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi 
Dk.Ali Mohamed Shein, akimuapisha Nd,Mussa Haji Ali, kuwa 
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi,
katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar,leo.

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,
(kushoto) akibadilishana mawazo na Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar 
Maalim Seif Sharif Hamad, na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ,
baada ya kuwaapisha Makatibu wakuu wa Wizara mbali mbali na 
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia Rushwa Zanzibar,katika hafla iliyofanyika 
Ikulu Mjini Zanzibar.


 Dk.Juma Malik Akili,Katibu Mkuu Wizara ya Miundimbinu na Mawasiliano



 Ali Khalil Mirza,katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Makaazi maji na Nishati


Mussa Haji Ali, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia Rushwa na 
Uhujumu wa Uchumi

Dk Shein awaapisha watendaji 

wakuu wa Serikali

Na Rajab Mkasaba, Ikulu

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. 
Dk. Ali Mohamed Shein leo amewaapisha baadhi ya Watendaji 
Wakuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar aliowateua hivi karibuni.
Katika hafla hiyo iliyofanyika Ikulu mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na 
viongozi mbali mbali wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dk. Shein 
alimuapisha Dk. Juma Malik Akili ambaye anakuwa Katibu Mkuu, 
Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano.

Aidha, Dk. Shein amemuapisha Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Makaazi, 
Maji na Nishati Bwana Ali Khalil Mirza pamoja na Bwana Mussa Haji Ali, 
ambaye anakuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia Rushwa 
na Uhujumu wa Uchumi.

Viongozi mbali mbali walihudhuria katika hafla hiyo akiwemo Makamu 
wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad, Makamu wa Pili wa Rais 
Mhe. Balozi Seif Ali Idd, Spika wa Baraza la Wawakilishi 
Mhe. Pandu Ameir Kificho, Waziri wa Nchi Afisi ya Rais na 
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Mwinyihaji Makame 
pamoja naMwanasheria Mkuu wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud.

Viongozi wengine waliohudhuria ni Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Utumishi 
na Utawala Bora Mhe. Haji Omar Kheir, Waziri wa Miundombinu na 
Mawasiliano Mhe. Rashid Seif, Waziri wa Ardhi, Makaazi, 
Maji na Nishati Mhe. Ramadhan Abdalla Shaaban, 
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdillahi Jihad Hassan, 
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe. Abdalla Mwinyi Khamis, 
Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar, Mstahiki Khatib Abdulrahman Khatib, 
Washauri wa Rais wa Zanzibar pamoja na viongozi wengine.

Mnamo Oktoba 15 mwaka huu Dk. Ali Mohamed Shein alifanya mabadiliko 
ya viongozi na watendaji wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kutumia 
uwezo aliopewa chini ya vifungu vya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.

Picha zote na Ramadhan Othman, Ikulu.

Chanzo: ZanziNews



No comments :

Post a Comment