Chama cha Wananchi CUF kimelaani vikali mno kitendo cha kumwagiwa tindi kali kwa Padri wa kanisa katoliki Cheju Zanzibar Anselmo Mwang’amba juzi jioni katika maeneo ya Mlandege, Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.
Mkurugenzi wa haki za binadamu habari uenezi na mawasiliano ya Umma Mh. Salim Bimani amesema kuwa matendo ya kihalifu yanazidi kuongezeka siku hadi siku ndani ya Zanzibar bila ya wahusika kukamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Amesema tukio hili la kumwagiwa tindi kali kwa Padri si la kwanza wala la pili huku jeshi la Polisi likiwa bado halijawashika wahusika wa matukio hayo ambao kwa makusudi wamekuwa na nia ya kuichafua Zanzibar kimataifa.Mkurugenzi wa haki za binadamu habari uenezi na mawasiliano ya Umma Mh. Salim Bimani amesema kuwa matendo ya kihalifu yanazidi kuongezeka siku hadi siku ndani ya Zanzibar bila ya wahusika kukamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Ameitaka Serikali SMZ kupitia Jeshi la Polisi kuhakikisha kuwa wanafanya kila jitihada za kuwakamata wahusika na hatimaye kuwafikisha katika vyombo vya sheria ili sheria ichukue mkono wake na hatimaye kukomesha kabisa vItendo hivi vya kihalifu ndani ya Zanzibar.
Aidha amelitaka Jeshi la Polisi kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa ili waweze kuwashikilia waliohusika na tukio na sio kukamatwa wasiohusika jambo ambapo linaipelekea jamii kujenga picha mbaya na jeshi hilo.
Aidha Mh.Bimani ametoa wito kwa Wazanzibari wote wanaoipenda nchi yao kutoa ushirikiano wa kina kwa jeshi la Polisi ili kufanikisha kukamatwa kwa wahusika wa matukio haya ya kihalifu.
Chanzo: ZanzibariYetu
No comments :
Post a Comment