zanglassworks

AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, October 19, 2013

Wawili wauawa kikatili

NA MWANDISHI WETU

20th October 2013


Watu wawili mkoani hapa wameuawa kikatili mmoja kwa kuchomwa moto na mwingine kuchinjwa kama kuku.
Aliyechomwa moto anakadiriwa kuwa na umri wa miaka 25 baada ya wananchi kumtuhumu kuiba kuku wanne.
Kamanda wa Jeshi la polisi mkoani Shinyanga, Kamishina msaidizi wa polisi, Evarist Mangala, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa wananchi hao walimshambulia kijana huyo kwa kumpiga mawe, fimbo, marungu na kuuchoma mwili wake.
Katika tukio lingine Lucia Masunga (61), mkazi wa kata ya Kizumbi mjini hapa, aliuawa na watu wasiojulikana kwa kumchinja shingo na kusababisha kifo chake hapohapo.
Mwanamke huyo alivamiwa juzi majira ya saa 4 usiku akiwa nyumbani kwake wakati akijiandaa kula chakula cha usiku na ndipo alipovamiwa na watu wasiojulikana na kisha kumchinja shingo na kusababisha kifo chake.
Kamanda Mangala alisema chanzo cha mauaji ya tukio la kwanza ni marehemu kutuhumiwa kuiba kuku na katika tukio la pili jeshi bado linaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha tukio hilo.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

No comments :

Post a Comment