dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, September 9, 2014

Tani 14.3 za majongoo zasafirishwa nje

 
 
Na Laylat Khalfan
TANI 14.35 za majongoo ya pwani, zimesafirishwa  nje ya nchi kwa mwaka 2013.

Akizungumza na mwandishi wa habari ofisini kwake Maruhubi, Mkuu wa kitengo cha usarifu na ukuzaji wa masoko,Hamad Khatib, alisema kiwango hicho kimeshuka  ikilinganishwa na tani 21 zilizosafirishwa mwaka 2012.

Alisema sababu za kupungua usafirishaji majongoo ni upungufu wa mazao hayo kutokana na kuongezeka idadi ya wavuvi.

Alisema soko kubwa la majongoo ya Zanzibar ni Marekani,Korea, Honkong, Vietnam, Dubai na nchi nyengine za Ulaya.Kwa upande wake, Hashim Muumin ambae ni  Mtafiti wa mazao ya baharini, alisema majongoo yapo hatarini kutoweka kutokana na kuongezeka idadi ya wavuvi.

Aidha alisema ipo haja kwa serikali kuweka mikakati madhubuti  ili kuunusuru uvuvi huo.

Hata hivyo, alisema wameandaa mikakati ya kuzalisha vifanga vya majongoo na baadae kuyaweka katika sehemu yaliyopungua.

Chanzo: ZanziNews

No comments :

Post a Comment