dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, September 11, 2014

Wanaume wana haki ya asili - Nyangwine

Mjumbe wa Bunge la Katiba, Nyambari Chacha Nyangwine. Picha na Maktaba 
Na Daniel Mjema, Mwananchi

“Wanaume wana haki ya asili kuanzia kwenye biblia, ndio maana wanaambiwa wao ni kichwa cha familia. Sasa tunadaije haki sawa na wanawake?” alihoji Nyangwine.

Dodoma. Mjumbe wa Bunge la Katiba, Nyambari Chacha Nyangwine amewapiga vijembe wanaume wanaotaka haki zao ziingizwe kwenye Katiba.
“Wanaume wana haki ya asili kuanzia kwenye biblia, ndio maana wanaambiwa wao ni kichwa cha familia. Sasa tunadaije haki sawa na wanawake?” alihoji Nyangwine.
Mjumbe huyo alitaka wajumbe wenzake kupigania haki za msingi za wanawake kama usawa katika vyombo vya maamuzi ili ziingizwe kwenye Katiba.
Wiki iliyopita wajumbe walio wachache katika Kamati Namba Tisa ya Bunge, walipendekeza wanaume wanaopigwa na wake zao nao walindwe katika Katiba mpya.
Mapendekezo hayo yaliyowaacha hoi kwa kicheko, yaliwasilishwa na mjumbe wa kamati hiyo, Mbaraka Hussein Igangula kwa niaba ya wajumbe walio wachache.
“Kwa mfano kuna baadhi ya wanaume wamekuwa wakipigwa na wake zao na kunyang’anywa mali kutokana na sababu mbalimbali,” alisema na kuwafanya wajumbe kuangua kicheko.

No comments :

Post a Comment