dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, October 18, 2015

Lusinde anusurika kifo!

Mgombea ubunge kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Jimbo la Mtera, Livingstone Lusinde
Mgombea ubunge kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Jimbo la Mtera, Livingstone Lusinde (pichani) amenusurika kifo baada ya helikopta aliyokuwa akiitumia kwenye shughuli za kampeni kupata hitilafu na kusababisha kushindwa kupaa. 
Akizungumza na Nipashe, Lusinde ambaye pia ni miongoni mwa makada waliopo kwenye timu ya kampeni ya Mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli, alithibitisha ajali hiyo kutokea katika Kijiji cha Idifu, wilaya ya Chamwino, lakini hakuna maafa yoyote yaliyotokea.
Alisema kulikuwa na jumla ya abiria watano kwenye helikopta hiyo akiwamo rubani na viongozi wengine watatu wa CCM, Wilaya ya Chamwino.
Aliwataja abiria wengine kuwa ni Mwenyekiti wa jumuiya ya wanawake UWT, Wilaya ya Chamwino, Devotha Mbogoni, Katibu Mwenezi wa wilaya, Marietha Mkuya na Mwenyekiti wa Kata ya Mvumi Mission, Mathias Lusano.
“Tulikuwa tunafanya mikutano kwenye jimbo la Mtera na baadaye ningeondoka kwenda Iringa, Njombe na Ruvuma ndivyo ilikuwa imepangwa, kwanza nilitoka Dodoma mjini mpaka Mvumi na nimetoka Mvumi nimeenda Chinoje, nikafanya mkutano nikaruka kutoka Chinoje hadi Igandu,” alisema.
Alisema baada ya kutoka Igandu aliruka kwenda Idifu ambapo wakati wa kutua rubani wao akagundua tatizo na kutua mbali na watu na baada ya kumaliza mkutano wake ndipo ndege ikashindwa kupaa.
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment