Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, November 4, 2015

Mgombea urais AFP adai uchaguzi Zanzibar haukuwa huru, haki!

Mgombea urais wa Zanzibar kupitia chama cha AFP, Soud Said Soud
Mgombea urais wa Zanzibar kupitia chama cha AFP, Soud Said Soud,  amesema uchaguzi mkuu wa visiwani hivyo haukuwa huru na wa haki kwa  sababu kulikuwa na watu waliokuwa wakiingia vituo vya kupiga kura  wakiwa na karatasi za kura mfukoni na kupiga zaidi ya kura moja  kitendo ambacho kinyume na sheria. 
 
Aidha, mgombea huyo amemtaka Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein,  aondoke madarakani kwa madai muda wake wa uongozi kikatiba umefikia  kikomo Novemba 2, mwaka huu na badala yake iundwe serikali ya mpito  itakayoandaa uchaguzi mwingine.
 
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Zanzibar jana, Soud alisema  baadhi ya watendaji wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (Zec) ndiyo chimbuko  la kuchafuka kwa uchaguzi wa visiwa hivyo, baada ya kushindwa  kusimamia majukumu yao ipasavyo kwa kuweka mbele maslahi ya vyama  vyao badala ya taifa.
 
Alisema uchaguzi huo ulitawaliwa na mizengwe ikiwamo vitendo vya  udanganyifu, vitisho na mawakala kupigwa na kuvuliwa nguo wakiwamo wa  chama cha Tadea katika mkoa wa Kusini Pemba.Alisema katika kituo cha kupigia kura cha Madungu katika mji wa  Chakechake, kura zilizidi idadi ya watu waliokuwa wameandikishwa  katika Daftari la Wapigakura ambao ni 180 lakini baada ya kufungua na  kuhesabu kura zilifikia 350. 
 
Aidha, alisema Soud alisema baadhi ya mawakala walikamatwa wakiwa na  kura mifukoni wakiwa katika hekaheka za kutaka kutumbukiza kura  zisizo halali katika masanduku ya kura halali katika kituo cha  Chonga, mkoa wa Kusini Pemba. 
 
“Uchaguzi wa Zanzibar ulikuwa uchafuzi siyo uchaguzi, lazima urudiwe  kulinda misingi ya kweli ya demokrasia ambayo kila mwanademokrasia wa  kweli ataitetea,” alisema.
 
Alisema katika Jimbo la Wawi mkoa wa Kusini Pemba, taratibu  zilivunjwa baada ya masanduku ya kura kuchukuliwa kutoka chumba namba  nne na kuhamishiwa namba sita na kazi ya kuhesabu kufanyika bila ya  kuwapo mawakala wa vyama vingine. 
 
Vyama vitatu hadi sasa vimetoa msimamo wa kutaka uchaguzi kurudiwa  Zanzibar kati ya 14 vilivyokuwa vimesimamisha wagombea kikiwamo CCM,  AFP na ADC. Kutokana na mgogoro wa kikatiba ulioibuka, Soud alisema  Rais Dk. Shein anatakiwa kuunda serikali ya mpito itakayokaa  madarakani kwa muda wa miezi 18 ambayo itaandaa uchaguzi mwingine  pamoja na kuiongoza Zanzibar katika kipindi cha mpito kuelekea  uchaguzi huo.
 
Alisema serikali hiyo lazima ishirikishe vyama vyote vya siasa, watu  wanaoheshimika na jumuiya za kiraia ili kumaliza mgogoro wa uchaguzi  wa Zanzibar.
 
Alisema Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kifungu cha 28 (2), inaeleza  wazi kuwa Rais ataacha madaraka yake baada ya kumaliza miaka mitano  kuanzia tarehe alipokula kiapo cha uaminifu pamoja na kiapo cha kuwa  Rais wa Zanzibar.
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment