dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, December 15, 2015

Baraza ya Cuf yavamiwa

Chama cha Wananchi (Cuf)
Watu wasiojulikana wamevamia Baraza ya Jumuiya ya Madola ya Chama cha Wananchi (Cuf) na kuvunja mabanda na mabenchi ya kukalia, katika mtaa wa Michezani, Mjini Zanzibar.
 
Tukio hilo lilitokea juzi, saa 4:00 usiku, baada ya watu wasiojulikana wakiwa na silaha za moto kufika katika eneo hilo na kuanza kuvunja mabanda na mabechi ya kukalia.
 
Wakizungumza na Nipashe mjini Zanzibar jana, baadhi ya wakazi wa eneo hilo walisema watu wasiojulikana wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 20 waliovunja baraza hiyo kwa kutumia vyuma vya kuvunjia vitu vizito ikiwamo mitalimbo.
 
“Walipofika walianza kuvunja kibanda kinachotumika kutoa huduma za simu pamoja na fedha na kukipakia katika gari. Tuliwaona wakipakia seti ya televisheni katika gari waliyoitoa katika baraza hiyo,” alisema mmoja wa mashuhuda, Ali Hussen, mkazi wa eneo hilo.
 
Alisema walipomaliza kuvunja na kupakia vitu hivyo katika gari,  wakisindikizwa watu wenye silaha waliovaa kiraia na walipokuwa wakiondoka katika eneo hilo walikatakata  mapambo ya vitambaa vya Cuf.
 
Naibu Katibu wa baraza hiyo, Omar Mussa Makame, alithibitisha kuvamiwa huko na kung’olewa mapambo na picha zote za Maalim Seif.
 
Alisema wameripoti tukio hilo  Kituo cha Polisi Mwembe Madema, Zanzibar na kwamba ni la pili kutokea katika baraza hiyo tangu kuanzishwa kwake.
Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Mkadam Khamisi, hazikufanikiwa baada ya wasaidizi wake kueleza yupo katika shughuli za kazi nje ya ofisi.

CHANZO: THE GUARDIAN

No comments :

Post a Comment