dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Monday, November 5, 2018

Watoto wa Khashoggi watoka mwili wa baba yao!


Watoto wa Jamal Khashoggi wahimiza kupatikana kwa mwili wa baba yao kwa ajili ya kundaa mazishi ya heshma

Watoto wa mwanahabari Jamal Khashoggi alieuawa katika ubalozi mdogo wa Saudia mjini Istanbul Oktoba 2 waomba mwili wa baba yao kwa ajili ya kuandaa mazishi.

Salah Khashoggi mwenye umri wa miaka 35 na Abdullah Khashoggi wakiwa katika mahujiano katika kituo cha CNN wameomba mwili wa baba yao kwa ajili ya kaundaa mazishi ya heshima ambayo ni jambo  msingi kwa kila binadamu  pindi anapofariki.

Katika mahojiano hayo, watoto wa Khashoggi wamesema kuwa hawatoweka matanga ya kifo cha baba yao wala kuacha kufuatilia sakata hilo iwapo hawatopewa mwili wa baba yao.

Salah amesema kuwa wanataraji kumzika baba yao katika makaburi ya familia ya al Baki mjini Madina.

Mtoto huyo wa Khashoggi amesema kuwa watu wanadhani kuwa wanayotaarifa kuhusu kifo cha baba yao ni kusema kwamba wao pia wanazipata taarifa kupitia vyombo vya habari.

Mtoto huyo alisema kuwa  baba yao alikuwa akitaraji kuanza maisha mapya nchini Uturuki ili kuwa karibu wa watoto wake.

Salah amesema kuwa picha zilizoonekana akisalimiana na mwanamfalme wa Saudia Mohammed bin Salman zimetafsiriwa  kinyume.

No comments :

Post a Comment