WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar na Riziki Pembe Juma ameitaka bodi mpya ya Ushauri ya Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu, kufanya Kazi kwa kufuata Sheria za Bodi hiyo ili kuleta maendeleo katika Elimu.
Amesema sheria zimewekwa kwa malengo ya kuongoza na kutenda haki, hivyo ni vyema kuitumia kwa kuleta mafanikio na kuacha muhali katika kutenda haki.
Akizungumza wakati alipozindua bodi hiyo katika ukumbi wa Wizara ya Elimu Mazizini Mjini Unguja, Mhe Riziki amesema maamuzi wanayoyatatua ni lazima kuyafikisha kwake ili kuyapitisha na endapo yatakuwa ni mazito yaweze kufikishwa Serikalini.
Amesema sheria zimewekwa kwa malengo ya kuongoza na kutenda haki, hivyo ni vyema kuitumia kwa kuleta mafanikio na kuacha muhali katika kutenda haki.
Akizungumza wakati alipozindua bodi hiyo katika ukumbi wa Wizara ya Elimu Mazizini Mjini Unguja, Mhe Riziki amesema maamuzi wanayoyatatua ni lazima kuyafikisha kwake ili kuyapitisha na endapo yatakuwa ni mazito yaweze kufikishwa Serikalini.










































