ZANZIBAR NI KWETU

Hili blog ni kuhusu Tanzania na dunia nzima kwa ujumla. Pita kila siku kwa habari moto moto.       (This blog is about Tanzania and the world as a whole. Pass-by everyday for breaking news). ***********************KARIBUNI NYOTE / YOU ARE ALL WELCOME!***********************

AirFreight

AirFreight

Kwarara Msikitini

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Monday, November 30, 2015

Mfuko wa kumsaidia mke, mtoto wa Mawazo kuanzishwa

Edward Lowassa akiaga mwili wa marehemu Alphonce Mawazo.
By Aidan Mhando na Salum Maige, Mwananchi.
Busanda. Mwili wa aliyekuwa, Mwenyekiti wa Chadema mkoani Geita, Alphonce Mawazo (Savimbi) umezikwa leo saa tisa alasiri kijijini kwao Chikobe Jimbo la Busanda mkoani Geita nyumbani kwa mjomba wake, huku simanzi, vilio na majonzi vikitawala.
Katika mazishi hayo, Mwenyekiti wa Chadema taifa, Freeman Mbowe alisema, ilikumuenzi Mawazo Chadema wataanzisha mfuko maalum utakao julikana kwa jina la Alphonce Mawazo Trust Fund, ili kumsadia Mtoto wa marehemu, Precious na Mama wa marehemu Hellena Gidioni,
Pia, Mbowe alisema,fedha zilizochangwa na wabunge wa Ukawa Sh33.9 milioni zitawekwa kwenye mfuko huo na michango mingine, huku akiahidi kuhuisimamia mfuko huo, ili usije kuleta mfarakano na utumike vizuri ilikumuenzi Mawazo.
Mazishi hayo yaliongozwa na  Mwenyekiti huyo wa Chadema  Mbowe,  Mawaziri Wakuu wa wastaafu, Edward Lowassa na Federick Sumaye, wabunge wa Ukawa na viongozi waandamizi wa chama hicho.
Mwili wa Mawazo ulitolewa nyumbani kwao saa 5:51 asubuhi, na kupelekwa kwenye uwanja Chikobe uliyopo mitata chache kutoka nyumbani kwao, huku mvua kubwa ikinyesha.
Aidha Mwili wa Mawazo ulibebwa na walinzi wa Chama hicho (Red Brigade) kutoka nyumani kwao hadi kwenye viwanja hivyo ambapo ibada ya kumuombea ilifanyika kuanzia saa 6:40 mchana.
Wakati wa utoaji wa heshima za mwisho kwa mwili wa mwanasiasa huyo, idadi kubwa ya watu hasa akinamama na vijana walionekana wakipoteza fahamu, huku wengine wakilia kwa sauti kubwa.

Read more »
at 6:06 PM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

CCM yakanusha taarifa za kuridhia kuapishwa kwa Seif

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai.
By Haji Mtumwa, Mwananchi
Zanzibar. Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimekanusha taarifa iliyosambazwa kupitia mitandao ya kijamii ya kuridhia Mgombea wa Chama Cha (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad atangazwe kuwa Rais wa Zanzibar.
Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake Kisiwandui mjini hapa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar, Vuai Ali Vuai, alisema wamepokea kwa msikitiko makubwa taarifa hizo alizoziita za uzushi.
 Alisema chama chake hakipo tayari kuvunja katiba wala sheria kwa kuridhia kuwa Maalim Seif atangazwe, kwani uchaguzi uliofanyika tayari umefutwa rasmi na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kupitia Gazeti la Serikali.
 "Mtandao huo wa kijamii ulidai kuwa mimi Naibu Katibu Mkuu niliwataka wananchama na wananchi wote kuridhia hatua hiyo iliyofikiwa ya chama chetu kuridhia kuapishwa Maalim Seif , huku nikisisitiza kwa kuwataka wananchi wote wajitokeze kwa wingi katika sherehe za kuapishwa rais", alisema Vuai.
Aliongezea kusema, "mbali ya hayo pia tarifa hizo zilinisingizia nimesema kwa kuwataka wananchi waridhie kuwa Dk Ali Mohamed Shein kuwa ni Makamo wa kwanza wa Rais wa Zanzibar mara bada ya kuapishwa kwa Maalim Seif kuwa Rais".

Read more »
at 6:03 PM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

MAGAZETINI LEO!


at 6:04 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

SHANTER SUGAR YAIFUFUA KIWANDA CHA MAHONDA!


at 6:02 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Mbunge wa Jimbo la Chumbuni Mhe Ussi Salum Pondeza AMJAD Awatembela Wananchi wa Jimbo lake wa Maeneo ya Masumbani, Chumbuni Kiungani na Chumbuni, Waliopata Athari za Mvua za Vuli Zinazoendelea Kunyesha Zanzibar.






Read more »
at 6:00 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Zanzibar promises investor friendly environment


PRESIDENT Ali Mohammed Shein has reiterated his government’s commitment to create more conducive environment for foreign and domestic investors.

He made the promise on Saturday during his visit to Mahonda Sugar Factory, north of Zanzibar Stone Town where he commended the ongoing refurbishing of the factory under the new management of ‘Shanta Sugar Holding Limited’ from India.

Dr Shein said the government recognizes efforts being taken by investors, as he assured that the government will continue to be close to both local and foreign investors for the development of the Islands.

“It is a fact that no country can develop without investors’ support because of their role in economy and providing employment to citizens,” said Dr Shein.

The more than $41m investment in the sugar factory has provided employment to at least 700 people comprising 200 working in the factory, and the rest in sugarcane farms.

Read more »
at 5:58 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Rungu la Magufuli latua kwa Bakhresa

Screen Shot 2015-07-16 at 8.18.52 PM*TRA yazuia makontena yake bandari kavu
*Polisi yasema uchunguzi mzito unaendelea
Dar es Salaam, MTANZANIA.
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imezuia kampuni ya Said Salim Bakhresa & Co. Limited kupeleka makontena yake katika Bandari yake Kavu (ICD), baada ya kugundulika kuwa baadhi ya makontena yalipitishwa bila kulipiwa kodi.
Kwa mujibu wa barua ya TRA ya Novemba 17, mwaka huu,  iliyosainiwa na Wolfagang Salia kwa niaba ya Kamishina wa Forodha na Ushuru wa Bidhaa, kampuni hiyo imezuiwa kutumia bandari yake hiyo- Namba 03 hadi kesi hiyo inayoshughulikiwa na mamlaka hiyo itakapotatuliwa.
“Unafahamu kwamba uondoaji wa bidhaa kutoka eneo linalodhibitiwa na forodha, ambalo kodi na ushuru wa serikali haujalipwa ni kinyume na sheria kwa mujibu wa Sheria ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Usimamizi wa Forodha ya mwaka 2004 na kanuni zake kwa vile husababisha upotevu wa mapato ya Serikali.

Read more »
at 5:53 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Chadema yateua Meya Manispaa ya Kinondoni

Pg 2Veronica Romwald na Ruth Mnkeni, Dar es Salaam, MTANZANIA.
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mkoa wa Konondoni, kimempitisha Diwani mteule wa Ubungo, Boniface Jacob (Chadema), kuwa mgombea umeya wa Manispaa ya Kinondoni, huku akiwakilisha mwamvuli wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
Mgombea huyo alikuwa akiwania nafasi hiyo huku akipambana na diwani mwenzake mteule wa Kata ya Mbweni, Abdunel Elibariki (Chadema) ambaye alishindwa kutamba.
Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo jana jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa uchaguzi huo Venus Kimei ,  alisema Jacob alishinda kwa kura 20 kati ya kura 28 zilizopigwa.
“Wagombea walikuwa wanne lakini watatu ndio ambao walikidhi vigezo, hata hivyo waliopigiwa kura ni wawili kutokana na mgombea mmoja Ndeshukurwa Tungaraza ambaye ni Diwani mteule wa Kata ya Makongo kujitoa katika hatua za mwisho,” alisema.

Read more »
at 5:50 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Almasi adimu yagundulika Tanzania

Omar-ChamboDar es Salaam, MTANZANIA.
KAMPUNI ya madini ya Petra Diamonds imegundua aina adimu ya almasi ya rangi ya pinki yenye uzito wa karati 23.16 kutoka mgodi wake wa Williamson uliopo Mwadui, Shinyanga.
Kwa mujibu wa taarifa ya kampuni hiyo ya madini, almasi hiyo ya pinki, moja ya madini ya rangi yanayosakwa zaidi duniani ni mfano wa ubora wa hali ya juu na ugunduzi mkubwa na muhimu zaidi kufanywa na Petra kutoka mgodi huo hadi sasa.
“Almasi za pinki hupatikana katika migodi michache duniani na uadimu wake huzifanya kuwa moja ya madini yenye rangi yanayotafutwa zaidi duniani,”taarifa ya kampuni hiyo ilisema.
Rangi ya pinki katika almasi inadhaniwa kuletwa kutokana na mabadiliko ya muundo wa molekuli, ambao unaaminika kusababishwa na aina fulani ya mtikisiko wa ardhi (seismic shock) unaotokea wakati wa kipindi cha uumbaji wa almasi.
Pande hilo la almasi litauzwa katika mnada huko Antwerp nchini Ubelgiji Desemba mwaka huu.

Read more »
at 5:48 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

….Watanzania tuombeeni Mungu-Majaliwa

Kassim+PHOTONa Mwandishi Wetu, Dar es Salaam, MTANZANIA.
WAZIRI Mkuu Majaliwa Kassim, amewataka Watanzania wamuombee kwa Mungu yeye pamoja na Serikali ya awamu ya tano chini Rais Dk. John Maugufuli, ili waweze kufanyakazi ya ukusanyaji wa mapato yatakayowanufaisha watu wote.
Majaliwa amesema watu wanaoamini kwamba hawawezi kufanyakazi kwa ajili ya kuliokoa Taifa waondoe dhana hiyo, kwani Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuhakikisha kila kinachokusanywa kama mapato ya nchi kinatumika kwa masilahi ya Watanzania wote na si kwa manufaa ya wachache.
Kauli hiyo ameitoa jijini Dar es Salaam jana katika ufungaji wa maadhimisho ya miaka 20 ya Dayosisi ya Pwani ya Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT) kwenye ukumbi wa PTA, viwanja vya Mwalimu Nyerere.
“Wako watu wanaoamini kwamba hatuwezi, nawaomba waondoe hiyo dhana. Wako watu wanaodhani kwamba utawala huu ni wa watu wapole, nao pia waondoe hiyo dhana.
“Tunawaomba Watanzania wote mtuunge mkono kwenye vita hii na mtuwezeshe kuifanya kazi hiyo. Tunaomba waumini wote mtuombee katika sala zenu za kila siku ili tuweze kuongoza kwa haki na kuwaletea Watanzania wote maendeleo,” alisema.

Read more »
at 5:46 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

HONDOHONDO : Magufuli anajijenga yeye, ataumbua wengi


By Joster Mwangulumbi

Sitaki umbea wala kuumbua watu. Miaka yote zikifanyika sherehe za Uhuru na nyinginezo, wasomi, wanasiasa na wananchi wa kawaida wamekuwa wakisifu maandalizi yake na kwamba zimefana. Hawakosoi.
Leo watu haohao wanamsifu Rais John Magufuli kwa kufuta baadhi ya sherehe hizo. Magazeti yanasifia tu. Fungua gazeti lolote huwezi kukosa vichwa: “Kasi ya Magufuli yatanda kila kona;” “Magufuli usipime;” “Magufuli atisha;” “Magufuli…” Hivi amefanya nini kipya, kufuta safari za nje? Je, amefuta safari au hali ya fedha inamlazimisha aangalie maeneo fulani ya kipaumbele?
Mtangulizi wake, Jakaya Kikwete alikuwa anajisifu, Magufuli anatenda ili wengine wamsifu. Ndiyo maana mara anatangaza kufuta ziara na sherehe, mara kavamia Hazina, Muhimbili, mara mikutano serikalini kufanyika kwa video, mara hakuna kuchapisha kadi kwa fedha za Serikali, mara amewamwaga vigogo TRA. Kesho yake magazeti yanampamba na kumjenga.
Ole wao watangulizi wake wadai kwamba anawaumbua! Ole wao CCM walalamikie kasi yake! Magufuli anajua watakaomnyoshea kidole watakumbana na nguvu ya umma.

Read more »
at 5:43 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

DARUBINI YA MTATIRO :Nchi hii haikuwa na kiongozi miaka 10 iliyopita?



Julius Mtatiro, Mwananchi.
Tangu
 Rais Pombe Magufuli alihutubie na kulizindua Bunge la Kumi na Moja Ijumaa Novemba 20, mambo kadhaa yamewashangaza wafuatiliaji wa masuala hapa nchini.
Mshangao mkubwa ulikuwa ni kwa namna Rais huyu mpya alivyokuwa anafafanua na kueleza uozo ulioko serikalini kama vile nchi haikuwahi kuwa na kiongozi kwa miaka mingi iliyopita.
Ni kama vile Tanzania ilikuwa ni kisiwa cha kuponda raha kuanzia Ikulu hadi kitongojini kwa mjumbe wa Serikali ya kitongoji, kijiji na mtaa. Yaani unaweza kustaajabu iweje nchi iendeshwe kwa udhaifu mkubwa namna hiyo na vyombo vyote muhimu vya dola vipo.
Sote tunafahamu kuwa hii ni nchi ambayo hata twiga na wanyama hai wengine husafirishwa kwa ndege kwenda nje ya nchi kinyume na sheria ya nchi yetu. Hii ni nchi ambayo wauzaji wakubwa wa dawa za kulevya wanaharibu maisha ya vijana wetu huku wanachekewa na kukaribishwa kwenye hafla kubwa za kuchangia hiki au kile.

Read more »
at 5:37 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

JPM aweka rekodi ya siku 25 ya mawaziri

Rais Dk John Magufuli
By Kalunde Jamal, Mwananchi
Dar es Salaam. Rais John Pombe Magufuli amekuwa wa kwanza tangu mfumo wa vyama vingi kuanza nchini kutumia muda mrefu kutangaza Baraza la Mawazi kutokana na kile wasomi, wachambuzi wa siasa kusema pengine anapata wakati mgumu kupata mawaziri watakaoendana na kasi yake.
Katiba ya mwaka 1977 inamtaka Rais kumteua waziri mkuu ndani ya siku 14 tangu alipoapishwa na kulipeleka jina lake bungeni, lakini katiba hiyo ipo kimya kuhusu uteuzi wa mawaziri, hivyo Rais anaweza kutumia muda wowote.
Wakati Rais mstaafu, Benjamin Mkapa alipoingia madarakani mwaka 1995 aliteua baraza la mawaziri Novemba 28, siku tano baada ya kuapishwa, Jakaya Kikwete alitangaza Baraza la kwanza Siku 14 baada ya kuapishwa na Dk Magufuli hadi sasa, siku 25 zimepita tangu aapishwe Novemba 5, mwaka huu hajafanya hivyo.
Kazi ambazo Rais Magufuli ameanza kuzifanya bila mawaziri ni kuzuia safari za nje, kuzuia sherehe za Uhuru na kuanza kupambana na wabadhirifu wa fedha za umma.

Read more »
at 5:32 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

TRA yaichunguza ‘bandari’ ya Azam

Mkurugenzi wa Mawasiliano na Elimu kwa Mlipa Kodi, Richard Kayombo.
By Nuzulack Dausen, Mwananchi.
Dar es Salaam. Mkakati wa kudhibiti uvujifu wa mapato serikalini unazidi kushika kasi baada ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuiagiza kampuni ya Bandari ya nchi kavu ya Azam kusitisha uhamishaji wa mizigo katika eneo la kampuni hiyo ili kupisha uchunguzi wa upotevu wa makontena na ukwepaji wa kodi.
Hata hivyo, uongozi wa Azam umebainisha kuwa upotevu wa makontena hayo hauhusishi bidhaa zinazomilikiwa na kampuni hiyo na kwamba umejitoa kwa hali na mali kufanikisha uchunguzi wa sakata hilo.
Kampuni hiyo inatuhumiwa kuhusika kwa upotevu wa makontena 349 yenye thamani ya Sh80 bilioni yaliyoripotiwa kupotea hivi karibuni wakati Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipofanya ziara ya kushtukiza katika Bandari ya Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa barua iliyoandikwa na Kamishna wa Forodha wa TRA, Wolfgang Salia kwa Meneja Mkuu wa Said Salim Bakhresa & Co Ltd, kampuni hiyo imezuiwa kupeka mizigo kwenye Bandari kavu namba 003.

Read more »
at 5:30 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Zitto: Lowassa alivuruga mipango yetu

Zitto Kabwe
By Joyce Mmasi, Mwananchi
Dar es Salaam. Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amesema nguvu ya aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa ilivuruga mpango wake wa kupokea wabunge 50 kabla ya Uchaguzi Mkuu.
Alisema Lowassa aliyekuwa akiungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) alikuwa na nguvu kubwa kiasi cha kufanya ACT pia ishindwe kupata wabunge wengi katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika nchini Oktoba 25.
Zitto alitoa kauli hiyo alipotakiwa kueleza sababu za ACT kushindwa kutimiza azma yake ya kupokea wabunge 50 kutoka vyama mbalimbali, kabla ya Uchaguzi Mkuu na kupata wabunge wengi baada ya uchaguzi huo kama alivyoahidi miezi michache kabla ya kuanza kwa kampeni.
Alibainisha kuwa chama chake kilifanya mazungumzo na wabunge wengi waliokuwa CCM na Chadema ambao walikubali kujiunga nacho na kushiriki uchaguzi kupitia chama hicho. Lakini mpango huo ulibadilika baada ya Lowassa kujiunga na Chadema na baadaye kuwania urais akiungwa mkono na Ukawa.

Read more »
at 5:27 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Mahakama yamuachia huru Sheikh Ponda

Sheikh Ponda Issa Ponda
By Hamida Shariff, Mwananchi Digital
Mahakama ya Hakimu mkazi mkoa wa morogoro imemwachia huru kiongozi wa taasisi na jumuiya za kiislam nchini sheikh ponda issa ponda baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha mashtaka yaliyofunguliwa mahakamani hapo dhidi yake.
Sheikh ponda aliachiwa huru na Hakimu mkazi mfawidhi Mary Moyo baada ya kukaa rumande kwa zaidi ya miaka miwili kutokana na kile kilichoelezwa kuwa dhamana yake ilizuiwa na mkurugenzi wa mashtaka DPP kwa maslahi ya taifa.
Akizungumza mara baada ya kuachiwa huru sheikh Ponda alisema kuwa anaishukuru mahakama kwa kutenda haki japo kuwa imechelewa na kwamba amekaa rumande tangu siku aliyokamatwa kutokana na dhamana yake kuzuiwa.
Katika kesi hiyo iliyovuta watu wengi wakiwemo waumini wa dini ya kiislamu sheikh ponda alikabiliwa na mashtaka mawili ambayo ni kutoa maneno yenye kuumiza imani za dini na kushawishi watu kutenda kosa ambayo alidaiwa kuyatenda agosti 10 mwaka 2013 katika viwanja vya shule ya msingi k.ndege manispaa ya morogoro.
Upande wa mashtaka katika kesi hiyo uliwakilishwa na wakili wa serikali mwandamizi Bernard Kongola, Sunday Hyera, na George Mbalassa wakati upande wa utetezi uliongozwa na wakili Juma Nasoro, Abubakar Salim na Batheromeo Tarimo.

at 5:24 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Serikali isiachie Coco Beach kumilikishwa kwa mtu mmoja.

NA EDITOR

30th November 2015.
Katuni.
Mahakama Kuu ya Tanzania, Kitengo cha Ardhi imeiamuru Manispaa ya Kinondoni kutekeleza mkataba wake na kampuni ya Q Consult inayomilikiwa na mfanyabiashara Yussuf Manji kwa ajili ya kuendeleza ufukwe wa Bahari ya Hindi kwenye eneo la Coco Beach, jijini Dar es Salaam.
 
Kutokana na hukumu hiyo iliyotolewa wiki iliyopita, endapo mwekezaji huyo atakamilisha taratibu za kulitwaa eneo hilo, wananchi na watoto wao waliokuwa wakitumia ufukwe huo kwa ajili ya kujiburudisha hawatakuwa na fursa hiyo tena, vinginevyo watalazimika kulipa kiingilio kitakachowekwa na mwekezaji huyo. Tunaomba na kuisihi serikali iingilie kati suala hilo na kuhakikisha kuwa eneo la Coco Beach linabakia kuwa eneo la wazi kwa ajili ya umma wa Watanzania.
 
Kampuni ya Q Consult ilifungua kesi hiyo kupinga kitendo cha Manispaa ya Kinondoni kusitisha mkataba wa kumiliki na kuendesha ufukwe huo. Hata hivyo, manispaa iliamua kuvunja mkataba ule kutokana na mwekezaji kushindwa kukamilisha masharti yaliyowekwa.
 
Tunapenda kueleza masikitiko yetu kwa kitendo cha ufukwe wa Cocoa kumilikishwa na mtu mmoja wakati inajulikana kwa miaka mingi ni eneo la wazi kwa ajili ya wananchi wote kujiburudisha.

Read more »
at 5:20 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Serikali yazungumzia tishio la Marekani.

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue.
Serikali imezungumzia tishio la Serikali ya Marekani la kusitisha misaada kwa Serikali ya Tanzania kutokana na mgogoro wa kisiasa Zanzibar na kukamatwa kwa maofisa wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu. 
 
Ofisi ya Ikulu jana ilisema masharti yaliyotolewa na Serikali ya Marekani yanatekelezeka na yatamalizwa kabla ya kikao cha Bodi ya Shirika la Maendeleo ya Milenia (MCC) kukaa Desemba, mwaka huu.
 
Wiki iliyopita, Serikali ya Marekani iliitaka Serikali ya Tanzania kumaliza haraka mgogoro wa kisiasa wa Zanzibar, vinginevyo upo uwezekano wa kusitishwa msaada wa zaidi ya Dola za Marekani milioni 472 (Sh. bilioni 999.4), za awamu ya pili ya fedha za MCC la nchi hiyo.
 
Fedha hizo za MCC awamu ya pili ni kwa ajili ya kuiwezesha Tanzania kusambaza umeme na kuwaunganisha wananchi wengi katika Gridi ya Taifa na uimarishaji wa taasisi zinazohusika na na sekta ya nishati.

Read more »
at 5:18 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Mawaziri Cuf sasa wadaiwa kulipwa mishahara bila kufanyakazi Zanzibar.

Rais Dk. Ali Mohamed Shein.
Wizara ya Fedha Zanzibar imesema mawaziri wa Chama cha Wananchi (Cuf) wanaounda Serikali ya Umoja wa Kitaifa (Suk), wanaendelea kupokea mishahara na marupurupu kama kawaida licha ya kujivua nyadhifa zao kwa madai utawala wa Rais Dk. Ali Mohamed Shein umefika kikomo Novemba 2, mwaka huu.
 
Hayo yalisemwa na Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Juma Ameir Hafidh, wakati akizungumza na Nipashe, visiwani humo mwishoni mwa wiki.
 
Alisema mawaziri hao wa Cuf na manaibu wao wamepokea mishahara na marupurupu ya mwezi Oktoba, mwaka huu licha ya kutangaza kujivua nyadhifa zao.
 
Alisema kwa mujibu wa kifungu cha 28 (1) (a) cha Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984, Rais Dk. Ali Mohamed Shein bado ni kiongozi halali hadi hapo Rais mpya atapochaguliwa na kuapishwa kushika wadhifa huo.

Read more »
at 5:17 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Makamanda UVCCM watakiwa kutokiangusha chama chaguzi.

Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka.
Makamanda wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), wametakiwa kuwa mstari wa mbele kukipigania chama chao na kuhakikisha  kinapata ushindi katika kila uchaguzi mkuu Tanzania Bara na Zanzibar. 
 
Akizungumza na makamanda wa UVCCM wa mikoa, wilaya, majimbo na wadi, huko Kilimani, mkoa wa Mjini Magharibi jana, Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka, alisema jukumu kubwa la makamanda hao ni  kupigana vita ya kisiasa na atakayeshindwa atakuwa ameshindwa kutumikia ukamanda  wake vizuri, hivyo kukiangusha chama.  
 
Alisema si jambo jema kwa makamanda kutoshirikishwa wakati wa uchaguzi, lakini pia si sawa wakajiweka nyuma wakati wa mapambano ya kutafuta kushinda uchaguzi ili kukamata dola. 
 
 “Nimekuiteni ili kuwakumbusha majukumu yenu, bila nguvu zenu, mipango na mikakati yetu ni vigumu kushinda vita iliyo mbele yetu, msibaki nyuma pambaneni hadi ushindi upatikane,” alisisitiza.
 
Aidha, Shaka aliwataka viongozi wa wadi, majimbo, wilaya na mikoa kuwapa ushirikanao makamanda hao, kwa sababu ndiyo wanaowajua vijana hodari, makini na shupavu wanaoweza kuhimili dhoruba za kisiasa wakati wa uchaguzi.

Read more »
at 5:15 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

MSD yaanza kudhibiti wizi wa dawa hospitalini.

Rais Dk. John Magufuli
Bohari Kuu ya Dawa (MSD) imeanza kuweka alama maalum kwenye vidonge 45 vya magonjwa ya aina mbalimbali  kudhibiti tatizo la wizi wa dawa nchini.
 
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa mwishoni mwa wiki, Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu, alisema vidonge hivyo vimewekewa alama ya GOT ambayo ni nembo ya serikali. Aidha, alisema tatizo la wizi wa dawa litadhibitiwa kutokana na  MSD kufanya kazi za uagizaji, uhifadhi  na usambazaji kwa kutumia mfumo wa mtandao wa E9. 
 
“Zamani ilikuwa tunaweka kwenye vifungashio vya ndani na maboksi alama ya MSD, lakini sasa hata kila kidonge kitawekwa alama ya GOT,” alisema.
 
Alizitaja baadhi ya dawa zilizowekewa alama hiyo kuwa ni Diclofenac, Amoxillin, Ciprofloxacin, Contrimoxale, Paracetamol na Magnesium.
 
Aidha, Bwanakunu alisema MSD itaanzisha huduma ya kutoa taarifa kwa njia ya simu pale wananchi watakapoona kuna wizi wa dawa za serikali na wataelimishwa namna ya kutoa taarifa pale wanapoona dawa za serikali mitaani.

Read more »
at 5:13 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Majaliwa: Kila kinachokusanywa kitatumika kwa maslahi ya wote.

Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim.
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim, amesema Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kuhakikisha kila kinachokusanywa kama mapato ya nchi kinatumika kwa maslahi ya Watanzania wote na si kwa manufaa ya wachache.
 
Waziri Mkuu alitoa kauli hiyo wakati akifunga maadhimisho ya miaka 20 ya Dayosisi ya Pwani ya Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT) kwenye ukumbi wa PTA, viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam jana.
 
“Serikali imeanza kukabiliana na upotevu wa mapato yake na kuepuka matumizi yasiyo ya lazima ya fedha za umma. Nia yetu ni kuhakikisha kila kinachopaswa kukusanywa kama mapato ya nchi, kikusanywe na kitumike kwa masuala ya msingi kwa ustawi wa Watanzania wote na si kwa watu wachache,” alisema.
 
Akifunga maadhimisho hayo kwa niaba ya Rais Dk. John Magufuli, Waziri Mkuu alisema serikali imedhamiria kupambana na maovu yote na kuondoa kero zinazowaumiza wananchi wa kawaida. 

Read more »
at 5:12 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Wafanyabiashara wahaha kumuangukia Dk. Magufuli

Rais Dk. John Magufuli.
Kuna taarifa kuwa moto wa Serikali ya Rais Dk. John Magufuli, katika kudhibiti ukwepaji kodi kwenye Bandari ya Da es Salaam, umezua taharuki ya aina yake kwa wafanyabiashara walioshiriki kuingiza kinyemela kontena 349 na kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya Sh. bilioni 80.
 
Taarifa zilizopatikana jijini Dar es Salaam jana zilieleza kuwa kufuatia uamuzi wa serikali kumsimamisha Kamishna wa TRA na kisha kumshikilia polisi na pamoja na vigogo wengine kadhaa wa mamlaka hiyo huku pia kukitolewa amri kwa wafanyabiashara wote walioingiza makontena hayo kulipa kodi mara moja kumeibuia hofu kubwa na tayari baadhi yao wameanza kujisalimisha kwa nia ya kumuangukia Rais Magufuli.
 
Chanzo kimedai kuwa hadi sasa, tayari baadhi yao wamekuwa wakihaha kwa kuwatumia watu mbalimbali wanaoamini kuwa wana ushawishi ili wawasaidie kumuonea Rais Magufuli kwa matumaini kuwa watapewa nafasi ya kulipa kodi waliyoikwepa na kisha kuachiwa ili waendelee na shughuli zao kama kawaida.

Read more »
at 5:11 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Lowassa, Mbowe, Sumaye watua alipouawa Mawazo.

Marehemu Alphonce Mawazo
Wakati mwili wa marehemu Alphonce Mawazo, ukitarajiwa kuzikwa leo kijijini kwao Chikobe, wilayani Geita, aliyekuwa mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kupitia Ukawa, Edward Lowassa, amewaongoza viongozi waandamizi wa chama hicho eneo alilouawa mwenyekiti huyo wa Chadema mkoani humo.
 
Msafara wa Lowassa ukiongozwa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye, wakiwa na wabunge zaidi ya 50 na wanachama na wafuasi wa chama hicho, walienda eneo hilo lililopo  jirani na makazi ya watu na kujioneo hali halisi.
 
Baada ya kufika eneo hilo alilouawa Mawazo, viongozi hao walisimika  bendera ya chama hicho pamoja na kuzungusha utepe mwekundu kuashiria sehemu iliyomwagika damu.
 
Baadhi ya watu baada ya kuliona eneo hilo walibubujikwa machozi, huku wakiamini kifo hicho kilipangwa kutokana na kushambuliwa eneo la wazi katika barabara kuu ya Geita - Katoro.
 
LOWASSA AMPONGEZA JAJI
Lowassa akizungumazana na waombolezaji katika viwanja vya Mnadani mjini Katoro, alimpongeza Jaji Lameck Mlacha wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza kwa kutoa uamuzi wa haki dhidi ya polisi waliozuia kuagwa kwa mwili wa Mawazo jijini Mwanza.

Read more »
at 5:09 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Njia tisa ukwepaji kodi Bandari Dar hadharani.

  Waliopitisha makontena kinyemela wahaha kumuona Magufuli Kampuni ya Bakhressa yakana kuhusika, watuhumiwa zaidi wanaswa Polisi.

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kodi Tanzania (TRA), Rished Bade
 Wakati Serikali ikikunjua makucha yake dhidi ya wote waliohusika katika kashfa ya kupitisha makontena 349 kwenye Bandari ya Dar es Salaam bila ya kuyalipia kodi, imefahamika kuwa idadi hiyo ya makontena ni sehemu ndogo tu ya mamia ya mizigo yanayovushwa kinyemela kila uchao na kuikosesha serikali mabilioni ya fedha.
 
Kuanzia mwishoni mwa wiki, serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk. John Magufuli imekuwa ikichukua hatua kadhaa za kukomesha ukwepaji kodi katika Bandari hiyo inayotegemewa zaidi kwa mapato nchini. Hadi sasa, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kodi Tanzania (TRA), Rished Bade, amesimamishwa kazi na kushikiliwa polisi kuhusiana na taarifa za serikali kukosa mapato takriban Sh. bilioni 80 kutokana na makontena hayo (349) kupitishwa bila ya kulipiwa kodi. Kadhalika, vigogo wengine kadhaa wa TRA wamesimamishwa kazi pia na kushikiliwa na polisi wakati uchunguzi zaidi kuhusiana na kashfa hiyo ukiendelea.
 
Hata hivyo, wakati serikali ya Rais Magufuli na Waziri Mkuu wake, Kassim Majaliwa, ikiendelea kutafuta suluhu ya kudumu kuhusiana na ukwepaji kodi, Nipashe imebaini kuwa kazi hiyo siyo lelemama kwani zipo njia zaidi ya tisa zinazotumiwa kukwepa kodi katika Bandari ya Dar es Salaam.
 
Uchunguzi wa Nipashe uliohusisha mahojiano na vyanzo mbalimbali umebaini kuwa wanaofanikisha ukwepaji wa kodi hushirikiana kupitia mtandao mpana unaohusisha wafanyabiashara wasio waaminifu, maafisa wa TRA, watumishi wa Bandari, wamiliki wa kampuni za usafirishaji na uondoaji mizigo, maafisa wa bandari kavu, maafisa wa benki zinazopokea malipo na pia baadhi ya askari. 

Read more »
at 5:07 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Sunday, November 29, 2015

MAGAZETI YA TANZANIA YA LEO!


at 11:36 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Chief Secretary stresses tough austerity actions

THE Chief Secretary (CS), Ambassador Ombeni Sefue

THE Chief Secretary (CS), Ambassador Ombeni Sefue, has challenged all civil servants to strictly implement the government’s orders on austerity cuts.

Ambassador Sefue said in a statement issued in Dar es Salaam yesterday by the Directorate of Presidential Communications, financial discipline must trickle down to all public offices. “President (John) Magufuli has shown us the way.

It is time for each executive to make personal evaluation on the degree of compliance to the directives on spending by ministries, departments and public institutions,” reads part of the statement.

In connection to financial control measures, Ambassador Sefue requested executive officers to reconsider importance in the publication, things like calendars, diaries and cards. “If there is need he or she should see the relevance and quantity to be ordered,” he noted.

Read more »
at 11:30 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Crackdowns on tax evasion win kudos

The Director of Policy and Research, Confederation of Tanzania Industries (CTI), Mr Hussein Kamote

TAX administration improvement measures taken by the government have widely won approval by some economists and other citizens who expressed hope for a new Tanzania.

Hardly a day after exposure of massive cheating by the Tanzania Revenue Authority (TRA) at the Dar es Salaam port following a surprise visit by the premier, Mr Majaliwa Kassim Majaliwa, interviewed financial experts have described the move as “timely and the right path towards self-sufficiency.”

The Director of Policy and Research, Confederation of Tanzania Industries (CTI), Mr Hussein Kamote, said tax evasion remained a long-time unresolved challenge despite voices by concerned parties.

“We (CTI) wrote and produced reports on massive cheating and losses of government revenue in trillions. We made it clear that re-establishment of local industries would have been a complicated process unless serious measures were taken to control importation of volumes of untaxed goods. “The government has now taken a commendable step to lift the country from a gridlock,” Mr Kamote commented.

Read more »
at 11:28 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Dar embassies prepare for challenges ahead


THE Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation has started implementing the decree issued by President John Magufuli banning all foreign travels by issuing specific instructions to its embassies abroad.

The ministry said in a statement released in Dar es Salaam yesterday that it had ordered all embassies around the world to get organised in order to participate fully in representing the government in all zonal and international meetings that will be taking place in the countries that they represent.

The statement further said that Tanzania has 35 embassies; three consulates; two business centres and 17 honorary consuls in different countries. It also stated that all these offices will be involved in forging ahead the country’s economic diplomacy and representing the nation’s interests abroad.


Read more »
at 11:24 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Tight security intensified at JNIA


IN a bid to ensure safety and security at the Julius Nyerere International Airport (JNIA), the aerodrome management plans to start screening all the parcels and other delivery by Tanzania Posts Corporation (TPC) at the airport.

The Director of JNIA, Eng Thomas Haule, made the revelation in Dar es Salaam over the weekend, stressing that the aim was to ensure tight security to customers, aircrafts and cargos.

“We are planning a thorough screening of all the deliveries by Tanzania posts, that means there parcels and other deliveries will be lined to be screened twice before being packed on aircraft for transportation,” he said.

He said the corporation has been criticised for involving in smuggling, transporting narcotics, ivory, bhang, among other prohibited items. “We have been receiving several mails from Holland and other areas, noting to have seized several parcels of narcotics, ivory, bhang among other controlled items from Tanzania,” he noted.

Read more »
at 11:21 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Ignorance fuels land conflicts in Z’bar


INEFFICIENCY in public offices and ignorance among citizens have been listed as some of the hurdles that continue to fuel land conflicts in Zanzibar.

“Most of us (particularly women in rural areas) do not have sufficient knowledge on our rights, yet staff in land commission have a tendency of not providing quick solutions,” said Ms Bahati Issa from Kikungwi village in South Unguja.

Ms Issa was among 50 women activists from villages who gathered at Kidongo-Chekundu psychiatric hospital function hall in Zanzibar municipality to discuss the impact of land conflict on women.

It was a gathering to mark the 2015 ‘sixteen Days of Activism against gender-based violence (GBV) campaign’ which started from November 25 and ends on December 10.


Read more »
at 11:19 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

WANANCHI WAANZA KUGAWANA (NGAWIRA) MALI ZA WAKUBWA WA TRA WALIOKAMATWA!

LATEST!
Inasemekana kuwa hizi nyumba zipo nne sehemu moja, tatu ndogo na moja kubwa. Huyo kijana anaeongea anaitwa Paulo Makasi Samjela na hivi sasa anatafutwa na polisi kwa kuingilia kazi yao na kuupotosha umma kwa kutumia social media.
  http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/979813-acheni-fitna-watanzania-bw-masamaki-tra-ni-tajiri-tokea-zamani.html#post14743383

MJUE BW. TIAGI MASAMAKI WA TRA!

http://michuzi-matukio.blogspot.ca/2014/11/tra-yaendelea-na-maadhimisho-ya-wiki-ya.html

 Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),Tiagi Masamaki akizungumza na uongozi wa Shule hiyo pamoja na wanafunzi kabla ya kukabidhi madawati,yaliyotolewa na TRA kwa shule hiyo.
 Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),Tiagi Masamaki akizungumza na wanafunzi wa darasa la kwanza wa Shule ya Msingi Misitu.
 Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),Tiagi Masamaki akipena mkoni na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Misitu,Hyasinta Hugo wakati akimkabidhi madawati 100 yaliyotolewa na TRA kwa shule hiyo.

at 9:59 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

TANI 332 WA CHAKULA NI MCHEZO MTUPU. NI SAWA NA TANI 100 ALIZOTOWA JK. WATU WATAKUFA NA NJAA VIJIJINI IRINGA!

Serikali yatoa tani 332 za chakula kijiji cha Mkukula




NA GEORGE TARIMO
29th November 2015.

Serikali imetoa tani 332 za chakula cha msaada kwa wanakijiji cha Mkulula wilayani Iringa wanaokabiliwa na upungufu wa chakula.

Aidha wananchi hao waliokuwa wakishindia ubuyu na matunda pori wamelalamika kuwa wanakula mlo mmoja kwa siku huku baadhi ya watoto wameshindwa kwenda shuleni.

Ukame uliotikisa baadhi ya vijiji vya wilaya hiyo umesababisha mazao kukauka, kwa mujibu wa maelezo ya wanakijiji waliyoyatoa kwa Mkuu wa Wilaya ya Iringa , Richard Kasesera.

Alifahamishwa hayo alipowatembelea na kuzungumza na wanakijiji cha Mkulula ambao ni waathirika wa njaa.

Japhet Mgimbuzi, akitoa kilio chake kwa Mkuu wa Wilaya alisema kutokana na hali mbaya ya hewa wanakula mlo mmoja lakini pia hawana fedha za kujikimu hali inayoongeza ugumu wa tatizo.


Read more »
at 9:33 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Serikali yakanusha kuhusu hazina kuachwa tupu!


Serikali imekanusha taarifa zinazosambazwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa Rais mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuwa amekomba fedha hazina na kuiacha Serikali bila fungu lolote.

Hayo yamesemwa jijini dare es salaam na Kamishina wa Bajeti kutoka Wizara ya Fedha Bwa. John Cheyo huku akiwataka wananchi kupuuza habari hiyo kwani hazina ukweli wowote.

Hazina inazo pesa za kutosha na tunajivunia kufanya uchaguzi wa mwaka huu, kununua mashine za BVR kwa kutumia pesa za watanzania bila kutegemea msaada wowote kutoka nje ya nchi na kutoa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu mwaka huu? alisema Bwa. Cheyo.

Pia aliongeza kuwa serikali imeendelea kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa bomba la gesi ambalo limekamilika hivi karibuni, vinu vya kuchakata gesi na ujenzi wa barabara nchini.

Aliendelea kusema kwamba mfumo wa serikali wa bajeti unaiwezesha serikali kupanga vipaumbele vya matumizi kulingana na bajeti ilivyopangwa ambapo fedha zinazokusanywa kupitia mfuko mkuu wa serikali ndizo hutumika.

Bajeti iliyoidhinishwa na Bunge kwa kipindi cha 2015-2016 ni shilingi Trilioni 22.5 na bajeti hiyo inatengenezewa mpango wa makusanyo na matumizi kwa kulipia mishahara ya wafanyakazi na miradi mbalimbali iliyoidhinishwa.

Pia katika matumizi mengine bajeti hiyo inalipia chakula cha wanafunzi, mikopo ya wanafunzi elimu ya juu, ununuzi wa dawa na vifaa tiba na chakula cha hifadhi ya taifa.

http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/978880-serikali-yakanusha-kuhusu-hazina-kuachwa-tupu.html 

at 9:20 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Ukwepaji Kodi: Barua ya TRA kwa Bakhressa

Mamlaka ya Mapato Tanzania imezuia kampuni ya Bakhresa kupeleka makontena yake katika bandari yake kavu.
Hii ni kutokana na baadhi ya makontena kugundulika kuwa yalipitishwa bila kulipa kodi.
http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/979583-ukwepaji-kodi-barua-ya-tra-kwa-bakhressa.html

at 9:11 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Trudeau's handshake scrutinized by international media

By Peter Henderson

By Peter Henderson | Canada Politics – Fri, 2



Justin Trudeau shaking hands with Queen Elizabeth II during a private audience at Buckingham Palace. (Photo by …

Prime Minister Justin Trudeau has been getting attention all around the word since his election last month. It’s not innovative foreign policy that’s making international headlines, but rather his good looks and youthful energy.

The day after his election, NBC News posted a story entitled “Meet Justin Trudeau: Canada’s Liberal, Boxing, Strip-Teasing New PM” that featured a shirtless picture of Canada’s new leader. The Daily Show’s Trevor Noah had a segment called “Canada’s Hot New Prime Minister,” but ironically the YouTube clip can’t be viewed from Canada. The UK Daily Mirror asked, “Is Justin Trudeau the sexiest politician in the world?”

Not everyone is a fan, however. On Wednesday the Daily Mail, a British tabloid known for its celebrity-obsessed coverage, suggested Trudeau had greets UK Prime Minister David Cameron with a “patronising” handshake when the two met for a bilateral discussion at 10 Downing St.

Trudeau had used both his hands to envelop Cameron’s right hand, which the tabloid suggested on its website is “politician’s handshake” that shows a lack of sincerity. Yet the paper didn’t miss the opportunity to post video of Trudeau stripping for charity in 2013.

Click here for a look at how Trudeau’s popularity has played out on social media.

at 9:07 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Nipashe ilivyoibua kashfa ya makontena bandarini

  • Kama uhujumu uchumi kupitia utoroshwaji wa makontena ulioripotiwa na gazeti hili mwaka jana ungefanyiwa kazi, vigogo wa Mamlaka ya Mapato (TRA) na Mamlaka ya Bandari (TPA) wasingekumbwa na kadhia ya kusimamishwa kazi.

Lakini licha ya matoleo matatu kuchapisha uozo huo kutokana na uchunguzi uliofanyika kwa weledi, mamlaka husika zilipuuza na badala yake zikakanusha ikiwa ni pamoja na kupitia matangazo yaliyolipiwa kutokana na fedha za umma. 

Ingawa habari hizo hazikuzungumzia moja kwa moja makontena yote 349 yaliyotajwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, lakini mwelekeo wake ulilenga kuonyesha namna vitendo vya ukwepaji kodi kupitia utoroshwaji wa makontena, vilivyokithiri nchini hususan ni kwenye bandari hiyo.

Moja ya habari hizo ni ile ya Juni 22 mwaka jana, gazeti hili lilipoandika habari yenye kichwa Makontena yaondolewa kinyemela bandarini Dar.
Makontena yaliyobainika kwa wakati huo yalikuwa ni pamoja na yaliyotokea China na kuondolewa bandarini kinyemela.


Read more »
at 8:57 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Makatibu Wakuu ofisini hakukaliki

  • Joto la utawala wa Rais John Magufuli limebadili utendaji kazi wa makatibu wakuu wa wizara mbalimbali waliozoea kukaa ofisini na sasa wanafanya kazi nje ya ofisi na kusikiliza kero za wananchi kwenye maeneo yao, Nipashe Jumapili limebaini.

Wakati hilo likifanyika, Ikulu jijini Dar es Salaam imesema katibu mkuu au mtumishi yeyote wa umma atakayeshindwa kwenda na kasi na mabadiliko ya utendaji kazi katika serikali ya awamu ya tano ajiondoe.

Tamko hilo linalotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, alipohojiwa jana kwa njia ya simu kuhusu kutokuwapo kwa makatibu wakuu wa wizara kadhaa kwenye ofisini zao wiki iliyopita. Uchunguzi wa Nipashe umebaini kuwa baadhi ya ofisi za viongozi hao kufungwa kwa maelezo kwamba wapo nje ya jiji kikazi.

Hali ya viongozi hao kuhama jiji na kwenda mikoani imeleta mabadiliko ya utendaji kazi wao baada ya miaka ya nyuma kuzoeleka kutumia muda mwingi ofisini na kuacha kazi za nje kufanywa na waziri, naibu au watendaji wengine.

Baadhi ya wizara ambazo zilitembelewa na kukuta ofisi za katibu mkuu zikiwa zimefungwa ni Uchukuzi, Tamisemi, Sayansi, Teknolojia na Mawasiliano na Ujenzi. 


Read more »
at 8:55 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest

Viongozi wa dini wataka Shein, Hamad kukubali matokeo ili kuunda SUK

  • Rais Dokta Ali Mohamed Shein na Katibu Mkuu wa  CUF, Seif Shariff Hamad ndiyo waliobeba amani na utulivu wa Zanzibar.

Viongozi hao ambao ni Rais na Makamu wake  wa kwanza, wanahimizwa kutenda haki na kuepuka kuukuza mgogoro wa Zanzibar ambao sasa umeanza kutishia mipango ya maendeleo ya taifa.

Wakuu hawa ndiyo wanaotakiwa kufahamu dhamana hiyo na  wasiwasikilize wapambe ambao mara nyingi hutazama  maslahi binafsi badala ya ustawi wa nchi.

Mgogoro wa Zanzibar wiki hii umetishia kuinyima Tanzania Shilingi trilioni moja (bilioni 999) zinazotolewa na Shirika la Changamoto za Milenia la Marekani (MCC).

Viongozi wa dini wakiwamo,  maaskofu na masheikh kutoka  Tanzania Bara na Visiwani na wa  mataifa wa Maziwa Makuu , wapo Zanzibar kuzungumzia mgogoro huo.

Wanasema  waamini kuwa jibu la amani ya Zanzibar ni Dk Shein na Hamad.

Wanawataka wawili hawa kuutendea haki Uchaguzi Mkuu uliofanyika  Oktoba 25,  2015 na kumtangaza  mshindi wa Urais wa Serikali ya Mapinduzi ya  Zanzibar (SMZ).

Jopo hilo  la viongozi wa kiroho wanaongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili , Amani  na Haki za Binadamu kwa Jamii ya Madhehebu, lipo Zanzibar kutathmin mgogoro huo.


Read more »
at 8:32 AM No comments :
Email This BlogThis! Share to X Share to Facebook Share to Pinterest
Newer Posts Older Posts Home
Subscribe to: Comments ( Atom )

Search This Blog

Click here to advertise with us!
Tweets by @znzkwetu

Books On Zanzibar Isles

Popular Posts

  • UAE's 47 billionaires control Dh598b wealth, says report! UAE's 47 billionaires control Dh598b wealth, says report!
  • Now perform Umrah throughout the year! Now perform Umrah throughout the year!
  • no image Vodacom launches 947m/- promotion
  • سورة الكهف كاملة (مكتوبة ) للقارئ الشيخ محمد الفقيه _ تلاوة خاشعة ومؤثرة😌💚 سورة الكهف كاملة (مكتوبة ) للقارئ الشيخ محمد الفقيه _ تلاوة خاشعة ومؤثرة😌💚
  •  Uganda’s Oil Journey: From Discovery to a Seat at the Global Decision-Making Table! Uganda’s Oil Journey: From Discovery to a Seat at the Global Decision-Making Table!

Pages

  • Contact us
  • Zanzibar Ni Kwetu Online Store
  • ZSSF PROJECT AT MBWENI, ZANZIBAR.
  • Advertise with zanzibar ni kwetu
  • MADUKA MAPYA YANAKODISHWA MWANAKWEREKWE, ZANZIBAR MKABALA NA MARIKITI!!!
online
Follow @znzkwetu

KITETE BEACH BUNGALOWS!

KITETE BEACH BUNGALOWS!

Shops for rent at Mwanakwerekwe, Znz

Shops for rent at Mwanakwerekwe, Znz

Shops for rent at Fuoni, Zanzibar!

Shops for rent at Fuoni, Zanzibar!

Zanzibar-Canadian Diaspora Association

Zanzibar-Canadian Diaspora Association
*************ZACADIA*************

****Zanzibar - Canadian Association****

****Zanzibar - Canadian Association****
*************ZANCANA*************

****Join the Zanzibar Ni Kwetu Team****

****Join the Zanzibar Ni Kwetu Team****

***The People's Bank of Zanzibar Ltd***

***The People's Bank of Zanzibar Ltd***
SEND MONEY FROM THE COMFORT OF YOUR HOME TO TANZANIA @ LOW FEES!

Zanzibar Properties

Zanzibar Properties

Visitors

Sparkline

Blog Archive

Copyright 2025. Zanzibar Ni Kwetu Blog. All Rights Reserved.. Powered by Blogger.