Hatua ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kutangaza nia ya kuwania Urais wa Jamhuri ya Muungano katika Uchaguzi Mkuu wa 2015, kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), imeibua siri nzito kuhusu uwezo na utendaji wake.
NIPASHE Jumapili limefanya tathmini ya tangu kushika wadhifa huo Septemba, 2, 2008, baada ya kujiuzulu kwa mtangulizi wake, Edward Lowassa, ambaye pia anatajwa kutaka kuwania Urais.
Wachambuzi wa masuala ya siasa wanamuelezea Pinda kwa namna tofauti zinazohusisha uwezo na upungufu wake katika kuishika nafasi hiyo, ikiwa atateuliwa na CCM na kushinda uchaguzi huo.
Miongoni mwa maeneo yaliyobainishwa katika utafiti huo kwa wiki nzima, ni pale Pinda, anapotajwa kuwa ni mwanasiasa asiyekuwa na ‘rekodi chafu’ katika utumishi wake wa umma, ama mwenye kashfa zinazohusishwa na uhujumu uchumi wa nchi au matumizi mabaya ya rasilimali na ofisi za umma.
NIPASHE Jumapili limefanya tathmini ya tangu kushika wadhifa huo Septemba, 2, 2008, baada ya kujiuzulu kwa mtangulizi wake, Edward Lowassa, ambaye pia anatajwa kutaka kuwania Urais.
Wachambuzi wa masuala ya siasa wanamuelezea Pinda kwa namna tofauti zinazohusisha uwezo na upungufu wake katika kuishika nafasi hiyo, ikiwa atateuliwa na CCM na kushinda uchaguzi huo.
Miongoni mwa maeneo yaliyobainishwa katika utafiti huo kwa wiki nzima, ni pale Pinda, anapotajwa kuwa ni mwanasiasa asiyekuwa na ‘rekodi chafu’ katika utumishi wake wa umma, ama mwenye kashfa zinazohusishwa na uhujumu uchumi wa nchi au matumizi mabaya ya rasilimali na ofisi za umma.















